Asalaam Aleikhum,

Ubalozi wa Tanzania Hapa London jana uliwaalika watanzania  kutoka madhehebu na dini mbalimbali kuja kupata futari ya pamoja walioandaa ikiwa ni ishara njema ya kuonyesha amani,upendo, ukarimu. 


Vyakula vya aina mbalimbali viliandaliwa  katika hadhi ya kitanzania. Naibu Balozi Mh Chabaka Kilumanga aliwashukuru wadau wote ambao walioweza  kujumuika na kufuturu kwa pamoja. 


Aidha Mh Kilumanga  aliahidi kushirikiana na watanzania kwa ukaribu zaidi kwa hali na mali pia kuwaomba kutoa ushirikiano wao na ubalozi katika kuboresha mawasiliano na utendaji wa kazi ili kusukuma mbele gurudumu la maendeleo. Aliendelea kwa kusema Ubalozi upo kwa ajili ya wote hivyo kila mtu na autumie ipasavyo.

Kwa niaba ya URBAN PULSE CREATIVE Tunapenda kutoa shukrani zetu za dhati kwa ubalozi wetu kwa namna walivyojitolea kutengeneza futari na kuwakaribisha wadau kuja kufuturu.

Asanteni Sana,

MUNGU IBARIKI AFRICA, MUNGU IBARIKI TANZANIA
URBAN PULSE CREATIVE
Waalikwa wakiomba dua baada ya kufuturu katika ubalozi wetu London, jana Jumamosi
Naibu Balozi Mh. Chabaka Kilumanga akitoa shukrani  na neno kwa waalikwa
Sehemu ya wageni
Afisa ubalozi Bw. Zamarani akikaribisha wageni kufuturu
Baadhi ya waalikwa kinama wakifuturu
Mkuu wa utawala na fedha ubalozini hapo Da'Carol Chipeta (shoto) akipozi 
na Da' Jestina George

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...