Wajumbe wa bodi ya taasisi isiyo ya kiserikali iitwayo SAVE MT. KILIMANJARO , bwana Ernest Olotu na Godlisten Mamba wakiwa nje ya viwanja vya Bunge la Jamhuri ya Tanzania mara baada ya kumalizika kikao cha bajeti ya Wizara ya mali asili na utalii pindi walipotembelea Bungeni hapo. Wadau hawa walipoulizwa juu ya ujuo wao Bungeni hapo, walisema ni katika harakati za kuelimisha umma wa watanzania ndani na nje ya nchi juu ya shindano la kusaka maajabu mapya saba ya asili ya dunia linaloendelea duniani kote na kushirikisha mlima kilimanjaro(Tanzania) na table mountains (South Africa) kwa upande wa Africa.Taasisi ya SAVE MT. KILIMANJARO ndio imeteuliwa na NEW 7WONDERS ,Kamati ya dunia ya kusaka maajabu hayo kusimamia elimu kwa umma na uhamasishaji wa kupiga kura kwa upande wa Tanzania.

Kwa kupiga kura tembelea; www.new7wonders.com au www.smk.or.tz

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Bongo hivi sasa watu wameshajua jinsi ya kula kiungwana!!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...