Mke wa Waziri Mkuu Mstaafu, Regina Lowasa pamoja na Mbunge wa Viti Maalum mkoa wa Arusha Namelok Sokoine wakicheza mziki wa Kwaito na Warembo wanaoshiriki shindano la Vodacom Miss Tanzania 2011, wakati wa tafrija maalum ya kuwakaribisha warembo hao katika mji wa Monduli juzi mkoani Arusha. Warembo wa Vodacom Miss Tanzania wapo Kanda ya Kaskazini kutembelea vivutio mbalimbali vya Utalii vilivyopo katika mikoa hiyo. 
Mke wa Waziri Mkuu Mstaafu, Regina Lowasa akicheza mziki wa Kwaito na Warembo wanaoshiriki shindano la Vodacom Miss Tanzania 2011, wakati wa tafrijka maalum ya kuwakaribisha warembo hao katika mji wa Monduli juzi mkoani Arusha. Warembo wa Vodacom Miss Tanzania wapo Kanda ya Kaskazini kutembelea vivutio mbalimbali vya Utalii vilivyopo katika mikoa hiyo. 
Baadhi ya warembo wanaoshiriki shindano la Vodacom Miss Tanzania 2011, wakiwa wamevalia vazi maalum livaliwalo na wanawake wa jamii ya Kimasaai wakati warembo hao na wenzao walipotembelea eneo la Snake Park mkoani Arusha jana. Warembo wa Vodacom Miss Tanzania wapo Kanda ya Kaskazini kutembelea vivutio mbalimbali vya Utalii vilivyopo katika mikoa hiyo. 
Warembo wanaoshiriki shindano la Vodacom Miss Tanzania 2011, wakipakua chakula wakati wa tafrija maalum ya kuwakaribisha katika mji wa Monduli jana. Tafrija hiyo iliyoongozwa na Mbunge wa Viti Maalum mkoa wa Arusha, Namelok Sokoine na dada wa Mbunge wa Monduli Kalaine Lowasa. 
Warembo wanaoshiriki shindano la Vodacom Miss Tanzania 2011, wakiwa katika picha ya pamoja na wenyeji wao baada ya kukaribishwa katika mji wa Monduli jana katika tafrija iliyoongozwa na Mbunge wa Viti Maalum mkoa wa Arusha, Namelok Sokoine na dada wa Mbunge wa Monduli Kalaine Lowasa
Dada wa Mbunge wa jimbo la Monduli na Waziri Mkuu mstaafu Kalaine Lowasa akiwavisha warembo wanaoshiriki shindano la Vodacom Miss Tanzania 2011, mgolole wa kimasai wakati warembo hao walipoandaliwa tafrija maalum ya kuwakaribisha katika mji wa Monduli.Kushoto ni Mbunge wa Viti Maalum Arusha, Namelok Sokoine. Warembo hao wapo Kanda ya Kaskazini kutembelea vivutio mbalimbali vya Utalii vilivyopo katika mikoa hiyo
Mbunge wa Viti Maalum mkoa wa Arusha, Namelok Sokoine akimshika mkono mmoja wa washiriki wa shindano la Vodacom Miss Tanzania baada ya kuvishwa mgolole wa kimasai na dada wa Mbunge wa Monduli, Kalaine Lowasa (wapili kushoto) jana baada ya kuwasili Monduli. Kushoto ni Mkurugenzi wa Lino International Agency, waandaaji wa shindano hilo, Hashim Lundenga
Baadhi ya warembo wanaoshiriki shindano la Vodacom Miss Tanzania 2011, wakiangalia nyoka aina ya chatu wakati warembo hao na wenzao walipotembelea eneo la Snake Park mkoani Arusha jana. Warembo wa Vodacom Miss Tanzania wapo Kanda ya Kaskazini kutembelea vivutio mbalimbali vya Utalii vilivyopo katika mikoa hiyo.
Mshiriki wa shindano la Vodacom Miss Tanzania 2011, Glori Lori akiwa amejivisha nyoka shingoni huku wenzake wakimwangalia wakati warembo hao na wenzao walipotembelea eneo la Snake Park mkoani Arusha jana. Warembo wa Vodacom Miss Tanzania wapo Kanda ya Kaskazini kutembelea vivutio mbalimbali vya Utalii vilivyopo katika mikoa hiyo.
Blessing Ngowi, Mshiriki wa shindano la Vodacom Miss Tanzania 2011, akiwa amejivisha nyoka shingoni huku wenzake wakimwangalia wakati warembo hao na wenzao walipotembelea eneo la Snake Park mkoani Arusha jana. Warembo wa Vodacom Miss Tanzania wapo Kanda ya Kaskazini kutembelea vivutio mbalimbali vya Utalii vilivyopo katika mikoa hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. THIS TIME WAREMBO WOTE NI WAZURI,MAJUDGE WATAKUWA NA KAZI YA ZIADA KUCHAGUA MSHINDI WA KWANZA.

    ReplyDelete
  2. 9c pics! bt i wz askin hamna pics zinazowaonyesha each miss tz in a poz!@ issa mchuzi

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...