MATAALAMU WA KAMPUNI YA GREEN FIELD YA HOLLAND Bw.  JOHN KRIMPEX AKIMUONESHA UBORA WA NYASI BANDIA BALOZI SEIF ALI IDDI MAKAMU WA PILI WA RAIS WA ZANZIBAR WAKATI ALIPOFANYA ZIARA YA GHAFLA KIWANJA CHA MICHEZO CHA GOMBANI KISIWANI PEMBA LEO.

Kazi ya  uwekaji wa Nyasi bandia  katika Kiwanja cha Michezo cha Gombani Kisiwani Pemba  zimeanza katika  hatua nzuri ya kuridhisha.

Uwekaji huo wa Nyasi unafanywa  chini ya usimamizi  wa Kampuni ya Ufundi ya Green Field kutoka Nchini Holland. Makamu wa Pili wa Rais   wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi amefanya ziara fupi ya ghafla kuangalia maendeleo ya uwekaji huo wa Nyasi Bandia.
Mtaalam wa  Kampuni hiyo ya Green Field  John Krimen alimueleza Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi  kwamba uwekaji  wa nyasi hizo unatarajiwa kukamilika rasmi mwishoni mwa mwezi huu.

John Krimen  amesema hatua ya awali ya utandikaji huo unaendelea kama program ilivyopangwa  ambao utachukuwa  kwa karibu wiki tatu kuanzia alhamis ya wiki hii.
Alisema mbali ya matumizi ya mchezo wa soka  katika Kiwanja hicho lakini pia nyasi hizo zinauwezo wa kuhudumia michezo mengine kama vile gwaride na Hlaiki na uingizaji wa magari ndani ya eneo la kati la uwanja huo ni kuhatarisha umadhubuti wa nyasi hizo.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi  amesifu juhudi zinazoendelea  kuchukuliwa na Wataalamu hao za kukamilisha kazi hiyo kwa wakati.
Balozi Seif amesema hatua hiyo itatoa fursa kwa wanamichezo kutumia kiwanja hicho katika mazingira ya kisasa zaidi.

Uwekaji wa nyasi Bandia katika kiwanja cha Michezo cha Gombani Pemba  ambazo zina uwezo wa  kutumika katika kipindi cha  karibu miaka kumi unasimamiwa na Shirikisho la Soka la Kimataifa FIFA kwa ushirikiano na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.  

Na Othaman Khamis Ame
Ofisi ya Makamau wa  Pili wa Rais wa Zanjzibar
9/9/2011.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...