Mwenyekiti wa Taasisi ya WAMA,Mama Salma Kikwete akiwapa nasaha vijana wa UVIKIUTA katika kituo chao huko Mbagala Charambe,Wilaya ya Temeke Mkoa wa Dar es Salaam leo alipowatembelea.kushoto ni Mwenyekiti wa UVIKIUTA, Ben Mongi.
 Mwenyekiti wa Taasisi ya WAMA,Mama Salma Kikwete akipatiwa maelezo na Mwenyekiti wa UVIKIUTA, Ben Mongi wakati alipotembelea katika kituo hicho kilichopo huko Mbagala Charambe.
 Baadhi ya vijana wa taasisi ya maendeleo ya vijana nchini wakisikiliza nasaha kutoka kwa Mwenyekiti wa Taasisi ya WAMA, Mama Salma Kikwete (hayupo pichani) alipotembelea na kuona shughuli za taasisi huko Mbagala wilaya ya Temeke. UVIKIUTA lengo lake ni kuwajengea uwezo vijana katika maeneo mbalimbali ya  kijamii na kuwawezesha kumudu maisha yao.
 Mwenyekiti  wa Taasisi ya WAMA,Mama Salma Kikwete akionyeshwa miche ya miti  mbalimbali na Mwenyekiti wa Taasisi ya maendeleo ya vijana (UVIKIUTA)  Ben Mongi (shati la kitenge) alipotembelea na kuangalia shughuli mbalimbali za taasisi huko Mbagala Mkoani Dar es Salaam.
Mwenyekiti  wa Taasisi ya WAMA,Mama Salma Kikwete akiwa kwenye picha ya pamoja na vijana wa Taasisi ya maendeleo ya vijana (UVIKIUTA) mara baada ya kukutana nao na kuzungumza nao huko Mbagala,mkoani Dar es Salaam.Picha na Mwanakombo Jumaa-MAELEZO.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Honera sana UVIKIUTA, mwanzo ulikuwa mgumu sasa mafanikio yanaonekana. UVIKIUTA ni mfano wa kuigwa na vijana, Hongera Ben na wote walioshiriki kuanzisha na kuendeleza UVIKIUTA. Doro.

    ReplyDelete
  2. hongereni ndugu zanguni wa UVIKIUTA. Nawatakia mafanikio zaidi na naamini matokeo mazuri kwa lolote mfanyalo.Big Up! wandugu

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...