Watanzania tunaoishi ujerumani tumesikitishwa sana na habari mbaya ya ajali ya meli iliyotokea 10.09.11 katika bahari ya hindi katikati ya visiwa vya Pemba na Unguja nchini Tanzania. Ajali hii ni pigo na msiba mkubwa kwa Taifa letu. Salam za rambirambi ziwafikie Familia za wafiwa, Viongozi wa Tanzania, na watanzania wote kwa ujumla.
Umoja wa watanzania ujerumani (UTU) kwa masikitiko makubwa tunaungana na wanafamilia, na taifa zima katika kipindi hichi kigumu cha maombolezo.
Tunatanguliza shukrani zetu za dhati kwa vyombo mbali mbali kwa jitihada zake za kuokoa maisha na kusaidia kwa namna moja au nyingine katka janga hili kubwa kwa Taifa


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...