UMOJA  WA  WANAFUNZI  WA  KITANZANIA  WASOMAO  KATIKA  CHUO  KIKUU  CHA  URAFIKI  (LUMUMBA) MJI  WA  MOSCOW  NCHINI  URUSI,  UNAPENDA  KUTOA  SALAMU  ZA  POLE KWA  WATANZANIA  WENZAO  KUFUATIA  AJALI  YA  MELI  ILIYOPINDUKA  NA  KUZAMA   KATIKA  VISIWA VYA  ZANZIBAR  MNAMO  SIKU  YA  JUMAMOSI  MAJIRA YA USIKU WA MANANE  NA  KUSABABISHA  VIFO  KADHAA VYA   ABIRIA WALIOKUWEMO  KATIKA  MELI  HIYO  WAKIWA SAFARINI KUTOKA UNGUJA  KUELEKEA PEMBA.

KWA  PAMOJA  TUNASEMA  MSIBA  HUU  NI  WETU  SOTE  NA  TUNAMUOMBA   MWENYEZI   MUNGU AWALAZE  MAREHEMU  MAHALA PEMA PEPONI,AWAPE SUBIRA WAFIWA NA AWAPE SHIFAA NA TAHAFIFU MAJERUHI NA WOTE WALIONUSURIKA NA KADHIA HIYO.
           KWAKE  TUMETOKA  NA  KWAKE  NI  MAREJEO.
                             AMEEN!!!!!!
             UONGOZI WA  WANAFUNZI-UWATA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...