RAMBI RAMBI KUTOKA KWA WATANZANIA TUNAOISHI HOUSTON KUFUATIA AJALI YA MELI YA MV SPICE ISLANDER.
Watanzania tunaoishi Houston, Texas, kwa masikitiko makubwa tunatoa rambi rambi zetu kwa Watanzania wote, na tunaungana na Taifa zima katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo.
Tunatoa pole zetu kwa waathirika, familia za wafiwa, na viongozi wa Taifa. Tunawaombea majeruhi wapone mapema.
Tunawashukuru wote walioshiriki na kuendelea kujitolea kwa hali na mali kuwasaidia walioathirika na ajali hii.
Mola awaweke pema peponi ndugu zetu waliotutangulia.
Novastus Simba.
Rais wa Jumuiya ya Watanzania Houston, Texas.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...