Meneja Miradi Maalumu wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Emma Oriyo akikabidhi kwa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi hundi ya Sh.milioni 10 zilizotolewa na kampuni hiyo kwa ajili ya kusaidia waathirika wa ajali ya Meli ya Mv.Spice Islander hivi karibuni.
Maofisa wa kampuni ya bia Tanzania wakimsikiliza Makamu wa Pili wa Rais wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi baada ya kukabidhi mchango wa sh. mil. 10 za kusaidia waathirika wa ajali ya meli ya MV. Spice Islander, mjini Unguja, Zanzibar mwishoni mwa wiki.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi akimshukuru Meneja Miradi Maalum wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Emma Oriyo (kulia), baada ya kupokea mchango wa TBL, wa sh. mil. 10 za kusaidia waathirika wa ajali ya Meli ya Mv.Spice Islander iliyotokea visiwani Zanzibar hivi karibuni.  (Wa pili kulia ni Mwakilishi wa TBL, Zanzibar, Mweidady Mbaga na Ofisa Uhusiano wa kampuni hiyo, Dorris Malulu.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi akisalimiana na Mwakilishi wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Zanzibar, Mweidady Mbaga baada ya kupokea mchango wa TBL, wa sh. mil. 10 za kusaidia waathirika wa ajali ya Meli ya Mv.Spice Islander iliyotokea hivi karibuni. Kulia ni Meneja Miradi Maalum wa kampuni hiyo, Emma Oriyo na Ofisa Uhusiano wa kampuni hiyo, Dorris Malulu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Kama wamekubali kupokea hizi pesa kutoka TBL basi wasivunje baa na wawaruhusu TBL kudhamini ligi na michezo mbalimbali huko Zanzibar.
    Michuzi cna nia mbaya usinibanie.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...