Mashabiki wakiwa katika msululu mreefu kuingia uwanjani.
 Baada ya kumejaa huku mchezo kati ya toto african na Simba ukiendelea mashabiki walilazimika kuvunja mlango wa kuingilia na kuvamia uwanjani huku baadhi yao wakiwa wameshikilia tiketi zao mikononi.
 Polisi walifanya kazi ya ziada kuwazuia na kuwarudisha. 
 katika tukio la kuvunja mlango wa uwanja kama kawaida waathirika hawakosekani ,kijana ambaye jina lake halikuweza kufahamika mara moja aliumia vibaya kichwani na hapa alikuwa akinawa eneo alilojeruhiwa.
 Tukio la aina yake ni pale mbwa wa polisi alipovamia uwanjani na kuanza kukimbiza wachezaji. 
 Hapa askari polisi akimtuliza mbwa aliyekuwa amemshikilia baada ya kuwakimbiza wachezaji katika uwanja hali iliyopelekea mchezo kusimama kwa dakika kadhaa.
Askari wa kikosi cha mbwa akiondoka na mbwa wake .Na Dixon Busagaga.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. Umenikumbusha zama zangu nakwenda Mao kupenya mpirani na huyo mbwa tulipa jina la Koplo John, heheheheeeeeeee!

    ReplyDelete
  2. duh! akina Ras Makunja na mbwa? kazi hipo

    ReplyDelete
  3. A very excellent blog post. I am thankful for your blog post. I have found a lot of approaches after visiting your post. 메이저사이트

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...