Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Sam Ellangallor
Airtel Tanzania imetangaza gharama mpya za kupiga simu Kenya na Uganda. Kupitia punguzo hilo wateja wa Airtel ndugu na jamaa zao sasa wataweza kufanya biashara kwa urahizi hasa zile zinazohusisha kuvuka mipaka ya nchi yetu na kuhusisha nchi za Kenya au Uganda kwa punguzo nafuu sana la Tsh 2.50 tu badala y sh 5 na sent 16

“Huu ni muendelezo wa kati ya dhamira endelevu tulizonazo Airtel kuwapa unafuu hasa wafanya biashara kuweza kufanikisha mahusiano yao kibiashara kati ya nchi moja hadi nyingine”

Akisisitizia Dhamira hiyo ya kupunguza gharama za mawasiliano kwa simu za kwenda nje ya nchi Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Sam Ellangallor aliendelea kusema “Airtel ni mtandao pekee unaotoa mawasiliano yenye uhakika zaidi kwa nchi za afrika mashariki. Airtel bado tutaendelea kuongoza kwa kutoa mawasiliano bora na kwa gharama nafuu zaidi tukiwa tunalengo thabiti la kuondoa kabisa changamoto ya mawasiliano katika nchi za Afika Mashariki”

Maendeleo ya uchumi wa jamii huwezeshwa na muunganiko wa jitihada au nyenzo nyingi, hivyo ninaimani kuwa kuvuka kwetu mpaka na kurahisisha mawasiliano ni dhairi itasaidia kukuza na kuboresha maisha ya jamii zote. Hili imewezeshwa zaidi na wateja wanaendelea kujiunga kila siku pamoja na dhamira yetu ya kutendelea kusambaa nchi za jirani” aliongeza kusema, Sam

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...