Mwakilishi wa UNESCO na Mratibu Mkazi mwakilishi wa Umoja wa Mataifa Vibeke Jensen akizungumza mbele ya Walimu na  Wanafunzi wa Shule ya Msingi Tandale ambapo shirika hilo limekarabati madarasa mawili ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya wiki ya Umoja wa Mataifa. Jensen amesema ni lengo la shirika hilo kuhakikisha Wanafunzi wanasoma katika Mazingira mazuri yatakayowawezesha kuwa na uelewa darasani. Katikati ni Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa UNIDO Bw. Emmanuel Kalenzi na Kulia ni Diwani wa Kata ya Tandale Jumanne Mbunju.
Afisa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa Tanzania Hoyce Temu akiwa na walimu wa Shule ya Msingi Tandale pamoja na wafanyakazi wenzake wa Umoja wa Mataifa wakipeana utaratibu wa kutekeleza kazi za kijamii shuleni hapo.
Afisa Habari wa UN Information Centre  Usia Nkhoma Ledama akitafsiri kwa lugha ya Kiswahili Hotuba iliyokuwa ikitolewa na Mwakilishi wa UNESCO na Mratibu Mkazi mwakilishi wa Umoja wa Mataifa  Bi.Vibeke Jensen.
Afisa Elimu wa Wilaya ya Kinondoni Hassani Kalinga (wa pili kushoto) akimkaribisha Mwakilishi wa UNESCO na Mratibu Mkazi mwakilishi wa Umoja wa Mataifa Vibeke Jensen (wa pili kulia). Kushoto ni Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Tandale Renatus Pallu na Kulia ni Diwani wa Kata ya Tandale Jumanne Mbunju.

Mwakilishi wa UNESCO na Mratibu Mkazi mwakilishi wa Umoja wa Mataifa Vibeke Jensen akionyesha mfano kwa vitendo wakati wa shughuli za ukarabati wa madarasa hayo.
 ukarabati wa madarasa ukifanyika.

Mwalimu Mkuu Msaidizi wa Shule ya Msingi Tandale Bi. Lucy Mwakibete akitoa shukrani za Shule kwa UN kwa niaba ya Mwalimu Mkuu Bw. Renatus Pallu ambapo ameshukuru Umoja wa Mataifa kwa ufadhili wa kukarabati sakafu za vyumba viwili vya madarasa kwa gharama ya zaidi ya Shilingi Milioni 3. Vilevile ametaja changamoto zinazoikabili shule hiyo ambapo amezitaja kuwa ni uchakavu wa Miundo mbinu, upungufu wa madawati, na ukosefu wa seti ya Kompyuta pamoja na mashine ya kudurufia.
 Baadhi ya wafanyakazi wa UN wakisililiza kwa makini hotuba ya Bi. Vibeke Jensen.
 Baadhi ya Wanafunzi wa Shule ya Msingi Tandale.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. tanzania bado tuko nyuma sana milioni tatu ni sawa na £1400 pesa hizi kama umetoa msaada sio lazima ukosanye watu wote ndio maana haya wenzetu wanatuona masikini sana wakati tz ni nchi tajiri tu inauma sana

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...