Waziri Mkuu Mizengo Pinda akiangalia moderm ya intaenti ya kampuni ya Vodacom wakati Meneja Mawasiliano wa kampuni hiyo Salum Mwalim akimpatia maelezo ya moderm hizo,wakati Waziri Mkuu alipotembelea banda la Vodacom katika maonesho ya bidhaa na huduma pembezoni mwa mkutano wa wadau wa uwekezaji eneo la ziwa Tanganyika unaofanyika Mjini Mpanda. Mkutano huo utafunguliwa kesho 17 Oktoba, 2011 na Rais Dk. Jakaya Kikwete.
Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Dk. Rajab Rutengwe akivutiwa na bidhaa mbalimbali za kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom katika banda la kampuni hiyo kwenye maoenesho ya wadau wa uwekezaji yanayofanyika mjini Mpanda. Mkutano huo unalenga kuongeza uwekezaji katika ukanda wa ziwa Tanyanyika unafanyika kesho 17 Oktoba, 2011 na utafunguliwa na Rais Jakaya Kikwete.Vodacom imegharamia chakula cha mchana na usiku kwa washiriki wa mkutano huo.
Meneja Mawasiliano wa kampuni ya Vodacom Salum Mwalim akimsikiliza kwa umakini kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa SACP Isunto Mantage wakati wawili hao walipokutana katika banda la Vodacom katika maonesho ya wadau watakaoshiriki mkutano wa uwekezaji katika ukanda wa ziwa Tanganyika mjini Mpanda. Mkutano huo unafanyika kesho 17 Oktoba, 2011 Mjini Mpanda, na utafunguliwa na Rais Jakaya Kikwete. Kampuni ya Vodacom imefadhili chakula cha mchana na cha usiku kwa wajumbe zaidi ya mia nne watakaohudhuria mkutano huo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...