Wachezaji wa Tume ya Kurekebisha Sheria (Tumesheria Sports Club) wakiwa wameshika bango wakati wa maandamano ya uzinduzi wa michuano ya SHIMIWI inayoendelea mkoani Tanga.
Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo Dr. Fenela Mukangara akizungumza wakati wa uzinduzi wa Mashindano ya Wizara na Idara za Serikali (SHIMIWI) mkoani Tanga
Mkurugenzi wa Kampuni ya ZP Bw. Zacharia Hans Poppe akipeana mkono na Mkuu wa Wilaya ya Tanga Bw. Ibrahim Msengi mara baada ya kutunukiwa Tuzo na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo Dk. Fenela Mukangala kufuatia kampuni yake kutoa mchango mkubwa uliofanikisha mashindano hayo (Picha zote na Ofisa Habari wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania Munir Shemweta)
Mkuregenzi wa Kampuni ya DP Shapriya Bw.Dipak Kotak akiangalia Tuzo aliyotunukiwa kwa kutoa mchango wa kufanikisha mashindano ya SHIMIWI ya mwaka huu, mwingine mwenye tuzo ni mwakilishi wa Kampuni ya Twiga Cement Bw. Mahmoud
Timu ya wavuta kamba wanawake ya Mambo ya Mambo ya Nje ikihangaika kujinasua ilipochuana na HAZINA ambapo katika mchezo huo timu ya HAZINA iliibuka mshindi
Wachezaji wa timu ya kuvuta kamba wanawake ya TUMESHERIA Sports Club wakiwa pamoja na Katibu Msaidizi na Mkuu wa Idara ya Utafiti ya Tume Bw. Adam Mambi (wa kwanza kulia) mara baada ya kutangazwa washindi dhidi ya Wizara ya Afrika Mashariki.
Baadhi ya wahisani wa Mashindano ya SHIMIWI ya mwaka huu wakiwa katika uzinduzi wa mashindano hayo, wa tatu ni mjumbe wa mashindano hayo Bw. Masubo.
Picha zote na Munir Shemweta.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...