Mkurugenzi Mkuu wa zamani wa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), David Mataka akitoka katika chumba cha Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam leo ambapo alisomewa jumla ya mashitaka matatu likiwemo la kushindwa kutoa taarifa sahihi za matumizi ya vitu mbalimbali vya shirika hilo.Bw. Mataka ameachiwa kwa Dhamana ya Sh. Mil. 20 kutoka kwa wadhamini wawili tofauti ambao kila mmoja amemdhamini kwa sh. Mil. 10.
Mkurugenzi Mkuu wa zamani wa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), David Mataka akisindikizwa na askari Polisi wakati akitoka kwenye chumba cha Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam leo alikosomewa mashtaka matatu likiwemo la kushindwa kutoa taarifa sahihi za matumizi ya vitu mbalimbali vya shirika hilo.Picha na Francis Dande wa Globu ya Jamii.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 23 mpaka sasa

  1. Hana hatia mwachieni! Si kawaida yenu?

    ReplyDelete
  2. Wa UDA naye lini atafikishwa kizimbani?

    ReplyDelete
  3. angetiwa ndani filauni huyu, masela wamuonje

    ReplyDelete
  4. Serikali msimhukumu mataka kwa kushindwa kuweka kumbukumbu za matumizi ya vitu. Jihukumuni ninyi wenyewe ambao mmeshindwa kuliendesha shirika hilo kibiashara hata kabla ya Mataka.

    ReplyDelete
  5. Pole sana Davi, ungekuwa unakula na kuchangia chama usingefikishwa hapo ulipo.

    ReplyDelete
  6. Huyu hausuiki moja moja na kuporomoka kwa shirika letu la ndege...

    ReplyDelete
  7. kwa suala la kupeleka wakubwa mahakamani JK anajitaidi tumpongeze kwa hili

    ReplyDelete
  8. Hali imebadilika siku hizi. Kigogo unaburuzwa mahakamani! Enzi za nanihii, unabadilishiwa post tu!

    ReplyDelete
  9. Kuburuzwa mahakamani ni one thing, nia ya dhati (kwa serikali) na hukumu ya HAKI (kwa mahakama) ni another!

    ReplyDelete
  10. da! how much money involved? vijisenti au?

    ReplyDelete
  11. katiba iweke kifungu cha kutokuwepo kinga yakushtakiwa Rais na viongozi wa juu ili nao waonje machungu ya utamu wao wakiwa madarakani

    ReplyDelete
  12. Duh kama siamini amini vile....mbona jamaa kajenga majengo ya ppf mawili, au na kule kachakaua nini mmmh....audit ipite tena ile ya PWC pale PPF....hueonda wakaibua mengi juu yake..

    ReplyDelete
  13. Pengine alikuwa anakula peke yake!!

    ReplyDelete
  14. Mie nafurahi kitu kimoja kwamba generation iliyopo na labda inayokuja hawapendi mafisadi. Wakiingia madarakani basi mafisadi wanalo..si mnaona kule misri..ni young generation!

    ReplyDelete
  15. Anon wa 04:43:00, ndiyo, kuburuzwa mahakamani ni one thing. Nayo ni hatua nzuri tu, Tena ni kubwa sana ukilinganisha na mtu akichafua sehemu anapelekwa kwingine na kuendelea kuchafua. Binafsi naiponeza sana serikali hii kwa angalau kuanza na hatua hii ya kwanza. Labda akina Mbowe wakiingia wataendeleza hatua ya pili na ya tatu (we hope!)

    ReplyDelete
  16. Alikula peke yake sana. Hebu angalieni maisha anayoishi na magari aliyekua nayo. Ile nyumba yake ya mbezi beach mnaijua wadau? Kama si mwizi hujengi kitu kama kile. Swali ni je? Haki itatendeka? Hakimu au mahakimu wana aminika?

    ReplyDelete
  17. Haki haitatendeka. Mahakama zetu tunazijua!

    ReplyDelete
  18. Huyu nae wanamuonea tu. Wanamtoa kama sadaka ili kujisafi.
    HE WHO HAS NO SIN, LET HIM CAST THE FIRST STONE!
    David, God will help you in this mess. We know they are dirty than you.

    ReplyDelete
  19. Wengi watakuwa wameumia ktk ATCL, hiyo PPF na kwingineko alikopita.... kwa udhamini wake wa kampuni ya mtandao, kwa kupenda watu wamwelekee kinyume nyume!

    Bosi amekuwa na tambiko ya ajabu sana!

    ReplyDelete
  20. Wengi watakuwa wameumia ktk ATCL, hiyo PPF na kwingineko alikopita.... kwa udhamini wake wa kampuni ya mtandao, kwa kupenda watu wamwelekee kinyume nyume!

    Bosi amekuwa na tambiko ya ajabu sana!

    ReplyDelete
  21. Safi sana, tena akatokomee huko jela na kundi lake, halafu mbona kosa limetajwa moja?Habari ya mahujaji je?Ndege ya Airbus iliyofilisi kampuni?ajira kimya kimya karibu watu mia, bila ya kutangaza.uozo ni mwingi

    ReplyDelete
  22. Hakuna uhakika kwamba eti kwa kuwa wewe ni kijana, basi hupendi ufisadi! kuna vijana/watu wengi ambao wanaonekana kutopenda ufisadi lakini mara tu wao wanapopewa nafasi hujikuta nao wakiendeleza ufisadi kwa kwenda mbele!

    ReplyDelete
  23. Ufisadi na fujo ni ugonjwa wa kudumu wa mtu mweusi kama anony mmoja hapo juu alivyosema. Leo huna wadhifa unajidai mwaminifu na kuwazomea wengine. Siku wewe ukipewa nafasi huwi fisadi ila nyang'au. Nyang'au ni mbovu zaidi ya fisadi maana nyang'au habakishi.
    Haya na tutoke nje ya mipaka yetu kidogo. Angalia mambo anayoyafanya jamaa mpya pale kwa Farao sasa hivi. Hata mwaka haujapita, anarudia makosa yale yale, yanayoweza kumfanya kesho ajute kuzaliwa. Hawa watu wanapokuwa kwenye viti wanakuwa wapumbavu au wanadhani wao ndiyo walioumba mbingu na nchi!

    Mara kwa mara nikimkumbuka Baba wa Taifa na kumfikilia saana, huwa simmalizi. Mzee yule alikuwa shuma mtupu walahi!RIP.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...