Mkurugenzi wa kampuni ya Afrikan Stars Enterteinment (ASET), Asha Baraka akionyesha moja ya CD feki za albamu ya Dunia Daraja mbele ya waandishi wa habari wakati akitangaza kuondoka kwa Bendi yake ya Twanga Pepepta inayotarajia kwenda nchini uingereza kwa shoo kadhaa.

Mwandishi wetu

BENDI ya muziki wa dansi ya African Stars “Twanga Pepeta International” itafanya onyesho kwa mara ya pili nchini Uingereza Jumamosi hii.

Akizungumza jijini Dar es Salaam leo, Mkurugenzi wa kampuni ya Afrikan Stars Enterteinment (ASET), Asha Baraka alisema kuwa jumla ya wasanii 13 wanatarajiwa kwenda huko kwa ajili ya kusherehekea miaka 50 ya Uhuru na Watanzania wahishio huko.

Baraka alisema, wanamuziki wao wanatarajiwa kuondoka Ijumaa na shoo itafanyika Jumamosi kwenye ukumbi wa Silver Spoon, Wembley bendi hiyo ikiwa huko itaendelea kufanya shoo zake kama kawaida nchini.

Mara ya kwanza kwa bendi hiyo kufanya shoo ilikuwa mwaka 2007 ambapo ilifanya shoo kwa wiki tatu katika miji mbali mbali mikubwa duniani.

Alisema, mgeni rasmi katika shoo hiyo anatarajiwa kuwa Balozi wa Tanzania wa Uingereza ambaye ni Peter Kallaghe na maandalizi yanaendelea vizuri ya safari hiyo.

“Kama unavyofahamika kuwa Tanzania tulitawaliwa na Waingereza na huko wapo Watanzania wanaohishi huko tumeona ni vyema tukaenda kuungana nao wenzetu kwa ajili ya kusherehekea miaka 50 ya Uhuru, alisema Baraka.

“Wasanii wanaoenda huko ni 13 na wengine watabaki kuendelea na shoo kama kawaida kwenye kumbi mbalimbali kwenye viwanja vya Leaders tutaungana na Msondo Ngom,” alisema Baraka.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Sasa yeye anategemea nini kama CD hazijasambazwa vya kutosha mitaani.

    Filamu wakitoa steps Jumatatu Dar Basi Ujue Mikoa mingine yote inaipata siku hiyo hiyo.

    Ye ametoa album ahalfu anasubiri waswahili wambembeleze kuuza wakati wanjanja wanasubiri kudurufu.

    Naomba umfikishie Ujumbe Huu.

    Kama anabisha apige simu Morogoro Leo aulize kama kuna duka lina cd / dvd yake.

    Kwa misingi hii, kuna uwezekano mkubwa wa kuuzika pirate mikoa mingine kabla ya original.

    Prince Sab.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...