Maafisa Vipimo wakiwa katika Picha ya pamoja mara baada ya Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi hiyo Bi. Magdalena Chuwa (wasita tokea kushoto waliosimama mstari wa mbele) Kufungua mafunzo hayo yaliyohusu taaluma mbalimbali katika tasinia ya Vipimo kuanzia tarehe 7.Mafunzo hayo yalikuwa ni ya wiki tatu kuanzia tarehe 7-25/11/2011 yaliyofanyikia katika ukumbi wa Dar es Salaam International Conference Centre. Mambo muhimu yaliyofundishwa kwenye training hiyo ni pamoja na uhakiki wa ujazo kwa vifaa mbalimbali mfano uhakiki wa ujazo wa sindano zinazotumika katika matibabu, uhakiki wa ujazo wa chupa za maji, uhakiki kipimo kinachotumika kupimia pampu za mafuta, uhakiki wa mizani za kupimia ujazo wa bidhaa mbalimbali , uhakiki usahihi wa Thermometer (kipimajoto) n.k.
Mtaalum toka nchi ya Jordan Eng. Osama Melhem akitoa mafunzo ya jinsi ya uhakiki usahihi wa Thermometer (kipimajoto) kwa washiriki wa mafunzo toka Wakala wa Vipimo ( WMA).
Maafisa Vipimo wakifanya mazoezi ya vitendo jinsi ya kuhakiki kipimo kinachotumika kupimia pampu za mafuta
Maafisa vipimo wakihakiki ujazo wa chupa za maji.
Afisa Vipimo akihakiki usahihi wa sindano inayotumika katika matibabu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...