Vodacom Tanzania inawashukuru wote ambao tayari wameshaonesha upendo wao kupitia kampeni ya “Red Alert” na kufanikisha kukusanywa shilingi 6,284,000/= kati ya December 22, hadi December 27, 2011.

Tunapenda kutoa wito wa kuendelea kuchangia Ndugu zetu waliopatwa na janga la mafuriko kwani bado wanahitaji misaada yetu,kwa Kupitia nambari ya Red Alert 15599 mteja anaweza kuchangia shilingi 500 kwa kutuma ujumbe mfupi – SMS wenye neno MAAFA na hakuna ukomo wa ujumbe na kwa njia ya m-pesa mteja anaweza kuchangia kuanzia shilingi 1,000 na zaidi kwenda nambari 155990.

Jinsi ya kuchangia kwa m-pesa

*150*00# kupata orodha ya huduma za m-pesa.

Hatua ya 2: Chagua 4 – Lipa Bili

Hatua ya 3: Weka namba ya kampuni – weka namba 155990

Hatua ya 4: Weka namba ya kumbukumbu – weka namba yako ya simu

Hatua ya 5: Weka kiasi – ni kuanzia Tsh 1,000 na kuendelea

Hatua ya 6: Weka namba yako ya siri

Hatua ya 7: Bonyeza 1 kwa kuhakikisha muamala na tayari utakuwa umeshachangia

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...