Marehemu Aziz Sheween (Kushoto) akiwa kwenye mazungumzo ya kikazi na Mwana wa Mfalme wa Saudi Arabia wakati wa uhai wake.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bw. John Haule, anasikitika kutangaza kifo cha Bw. Aziz Sheween, Afisa Mambo ya Nje Mkuu Daraja la I katika Ubalozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia, kilichotokea huko Riyadh, Saudi Arabia.

 Taratibu za kusafirisha mwili wa marehemu kuja nyumbani kwa mazishi zinaendelea na pindi zitakapokamilika taarifa rasmi itatolewa. Tunawapa pole familia ya marehemu, ndugu, jamaa, marafiki, watumishi wa Wizara na wote walioguswa na msiba huu mzito.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa
S.L.P 9000
Dar es salaam, Tanzania
www.foreign.go.tz

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 15 mpaka sasa

  1. Kiukweli nimesikitishwa sana na kifo chake ila ndo ahadi ya Mungu ikifika hatuna cha kufanya. Rest in peace bro.. Nawapa pole wanafamilia na nawaombea moyo wa subira poleni sana

    ReplyDelete
  2. Ni pigo kubwa kwa Wizara ya Mambo ya Nje na familia kwa kuondokewa na mfanyakazi hodari ambaye alikuwa ni hazina kubwa sana. Tunaomba roho yake ipumzike mahali pema peponi, AMEEN.

    ReplyDelete
  3. Am out of words.... Ntakukumbuka daima ndugu yangu. Bwana ametoa na bwana ametwa.... R.I.P Aziz.

    ReplyDelete
  4. Mungu amuweke mahali pema, ndio mapenzi ya mola. Mwenyenzi mungu awafariji familia ya marehemu.
    Leo umetutoka lakini ndio amri ya mola.Amina!

    ReplyDelete
  5. Jamani Bro Sheween! Alinisaidia sana nikiwa Foreign. Kaka nenda kwa amani. Ee Mungu ipe familia yake nguvu ya kulipokea na kulikubali pigo hili kubwa. Poleni sana wana-foreign! R.I.P Brother Aziz Sheween!

    ReplyDelete
  6. RIP Auncle Aziz! kifo chako ni cha ghafla umetuacha kwenye majonzi mazito, daima ucheshi,upendo wako tutavikumbuka daima, Mwenyezi Mungu akuweke mahala pema peponi Amina!

    ReplyDelete
  7. Pole sana Sophia Kawawa na watoto, Mungu awape subira kwenye wakati huu mgumu, Inalillah Wainalillah Rajun

    ReplyDelete
  8. kaka uende kwa amani, ila sitasahau wema na upendo wako kaka. ulimsaidia mtu wangu wa karibu alipokwama kwa kupoteza pasipoti yake. At that mtu wangu hakuweza kuthibitisha kama alikuwa Mtanzania, na hakuna mtu ubalozini (not in Saudi) aliyekuwa tayari kumsaidia pa kumhifadhi. Ila wewe ukajitolea kumhifadhi na ukamsaidia mpaka akaweza kuondoka salama. Ahsante sana kaka kwa msaada, sikuweza kukuona uso kwa uso kukupa ahsante yangu. Nashukuru sana. Mola aipe nguvu na amani familia yako katika kipindi hiki kigumu kwao. Once again, thank u! thank u! for being there for us at that difficult time for us. RIP bro Aziz

    ReplyDelete
  9. POLENI SANA NDUGU,MARAFIKI NA WAFANYAKAZI WOTE WA WIZARA YA MAMBO YA NJE.MWENYEZI MUNGU AMLAZE PEMA PEPONI -AAMIN.HE WAS A NICE YOUNG DIPLOMAT NA ALIKUWA RAFIKI WA KADA ZOTE BILA KUJALI YEYE NI NANI.SI WOTE WANAJALIWA KARAMA KAMA YA AZIZ.RIP BRO AZIZ.-ADAM

    ReplyDelete
  10. Rest in Peace, I do not know you but from the comments above you seemed to be a good person "mtu wa watu" Mwenyezi Mungu akufunulie nuru yake upumzike kwa amani, pole na wapate nguvu familia walio bakia. bll

    ReplyDelete
  11. Ni Kweli Bwana Azizi ni Mtu wa watu, mtu mzuri mtu mwenye ushirikiano na watu, habagui mkubwa na mdogo wa kihceo wala umri, nawapa pole wanafamilia ndugu jamaa na marafiki na hasa watumishi wa Ubalozi wa Tnzania Mjini Riyadh, kazi ya Mungu haina makosa yeye ndio mwenyekupanga na kuamua kile alichokipanga.. Innaa Lillah wa Innaa Ilaihi Raji3un..
    Abu Bintain

    ReplyDelete
  12. R.I.P Aziz. You will always be remembered for your kindness and charm.

    ReplyDelete
  13. rest in pace Aziz

    ReplyDelete
  14. R.I.P uncle Aziz. We will miss you.

    ReplyDelete
  15. Mungu amrehemu brother Aziz.

    Alikuwa ni binaadamu ambaye alikuwa hapendi kuona mtanzania anapata tabu ugenini. Sura yake ya ucheshi na uamuzi wake wa busara, tumeikosa...

    Watanzania tuliopo Riyadh tutam-miss sana Aziz.

    Mungu amrehemu na awape subra na imani family yake. Amin

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...