Binti yetu Zenna Ally Mapee mwenye umri wa miaka 22 amepotea nyumbani tangu tarehe 3/2/2012 aliaga anakwenda Mbagala na kisha kuelekea Mwananyamala kwa shangazi yake. Ni kawaida huwa anaenda na kurudi nyumbani. 

Alipiga simu akitujulisha kuwa atarudi usiku kwa kuwa ilikuwa usiku kama saa mbili hivi tulimwambia alale kwa Shangazi ili arudi kesho mapema. Tulikubaliana hivyo siku ya Ijumaa tarehe 3/2/2012 asubuhi kama saa tano alikuwa bado hajarudi tukapiga simu kwa Shangazi ndipo aliposhangaa kwani hata jana yake hakuwa huko. 

Tumejaribu kumtafuta kwa ndugu na jamaa bila mafanikio na kutoa taarifa vituo vya police bila mafanikio. Tunaomba mtu yoyote ambaye anataarifa za Zena awasiliane na sisi kwa simu tutazitoa hapo chini au hata kwa kupitia blog hii.

 Zena kama unaona tangazo hili na kwenye vyombo vya habari popote ulipo tunakuomba urudi nyumbani Familia zote za Mzee Iddi Sungura na Familia ya Mzee Mapee wote tunakupenda, tunakujali na tunakuhitaji sana.

Namba zetu za simu kwa taarifa.

0716 696858- Shangazi Mama Hadija
0713 400363 – Kaka Madaraka
0778 612613- Mama Mdogo Masha Sungura
0715 080926- Mama Mdogo Utesi Sungura
0656 369316- Mama Mdogo Shindo Sungura

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 34 mpaka sasa

  1. tangazo hili ungelipeleka TBC bango ingekuwa rahisi zaidi watu wengi wangemuona

    ReplyDelete
  2. suali dogo tu, mumejaribu kumpigia simu? i assume ana mobile na ndiyo alopiga kusema atarudi usiku. ni wazo tu. Inshaallah ataonekana na kurudi nyumbani kwa familia yake kwa salama amin

    ReplyDelete
  3. Poleni sana wazazi na watu wa karibu
    lakini kwa taarifa hizi msifadhaike huyo binti inaonyesha hajapotea wala kupata matatizo, ila kwakua anajiona kakua ameamua kuacha nyumbani kwao na kuenda kwake bila kufuata utaratibu rasmi.
    Kifupi ameenda kwa bwana!!¨hivyo wazazi kwakua mmekwishatoa taarifa tulieni atakuja mwenyewe tu akili ikimuingia.
    Angepata asingepiga simu na angekua amefika kwa shangazi yake, kosa mlilofanza bila kutegemea ni kumruhusu kulala kwa shangazi yake bila kuwasiliana nae, na sasa amenogewa.

    ReplyDelete
  4. huyo hajapotea kuna mtu kamuweka ndani kwa mda, nahisi anaona aibu kurudi ngojeni ajipange kuja kuwadanganya!

    ReplyDelete
  5. Mashaallah!! Binti wa haja hasa.
    Jamani wanaume wenzangu, yeyote aliyepiga bao la kisigino hapo hajakosea wala kulaumika. Tuwasiliane ili niwe mshenga na tuhalalishe maisha ya huyu binti huko aliko.
    Hakika ni mpini wa nguvu, hivyo tusiwasumbue Wazazi wake bure.

    Abiola Jr.
    Mafia kiduka cha juice

    ReplyDelete
  6. Huyo hajapotea, msichana wa umri wake huwa hapotei ila anachelewa kurudi tu. Ondoeni shaka.
    Ana hamu ya kupika chungu chake sasa na anaonekana dhahiri kuwa 'mapishi" anayajua.

    Ignas wa Chelsea

    ReplyDelete
  7. Nadhani, atakuwa amepata mume,na sasa nahisi ni mshenga ndiye atakayejitokeza ili awaambie msimtafute binti yenu tunaye.

    ReplyDelete
  8. Sura hii haiwezi kulala bus stand. Kuna malazi mazuri yameandaliwa kwa ajili yake. Wazazi wavute subira. Watajua alipo. Ana mvuto binti huyu, bwana.

    ReplyDelete
  9. Tatizo mnawafungia sana nao huwa wanatakiwa kusevisi maungo.

    ReplyDelete
  10. Fedheha inayofanywa hapa ni ya kusikitisha. Ni busara kuwaonyesha wazazi hawa na ndugu wenye hofu na upendo wa ndugu yao huruma wanayostahili badala ya kejeli za kipuuzi.

    ReplyDelete
  11. poleni wazazi wenzangu, hawa watoto wa kike wanamatatizo yao. kama alipga cmu nipo kwa shangazi hali ya kuwa hayupo, basi kwa imani yangu yupo kwenye mikono salama ya dhambi, ninachomuomba binti rudi home halafu uondoke kweupe na siyo kututesa ss wazazi tuje kupata pressure hali ya kuwa wadogo zako ni wadogo.

    ReplyDelete
  12. Hawa ndio watoa maoni wanaohitaji Taifa liendelee na ndio tunaowategemea kwenye maoni ya katiba mpya, inakuwaje kuanza kumtolea binti wa watu maneno makali kiasi hicho na hakuna lolote mlilothibitisha.Tuna ndugu zetu, jamaa au marafiki wangapi waliopotea kwenye mazingira ya kutatanisha?, Je ni wangapi tulioletewa taarifa kupatikana maiti zao baada ya kupotea?. Sidhani kama hapa panatembelewa na watoto wa shule za msingi na hata kama wapo wa sekondari ni wachache sana, naomba tujitahidi kuandika maoni kutokana na umri na upeo tulionao na si kukurupuka na hoja zisizo na uthibitisho.. Siwatakii mabaya ila yatakapowakuta kwa watoto, wazazi au ndugu zenu ndio mtaelimika zaidi na kujifunza kuongea mbele ya jamii linapotokea tatizo.. Mungu amuongoze na amuepushe na madhara yote yaliyo na yanayo msibu huko alipo.


    Kijana Mdogo

    ReplyDelete
  13. Poleni Wazazi kwa kuzidiwa akili na Kachala!

    Inaonekana mchezo huo aliuanza kipindi na sasa amenogewa kama Wadau walivyo tutaarifu kwa Maoni hapo juu.

    Mara nyingi kwa Taratibu za Malezi haifai mtoto wa Kike au Binti aliye ktk umri kama huo au Mtoto aliye chini ya Mamlaka kutoka safari bila kushindikizwa!

    Inatakiwa wawepo zaidi ya angalau wawili na lazima ijulikane watapita wapi na watarudi muda gani.

    Zaidi ya hapo Wazazi au Walezi mlitakiwa KABLA msome nyendo zake Binti na kama mngebaini ameshajitambua amekuwa mtu mzima ni bora mngembana amlete huyo Kachala muwape Mamlaka wa kuwa Mume na Mke kwa njia Halali!


    Muharibifu Kachala ametumia mwanya huo wa upungufu wa Usimamizi na sasa amepiga Bao ametulia na mwanamke wa bure kwake Mbagala!

    ReplyDelete
  14. Hajapotea,,,kwa umri wake ni kuwa ameshapata 'Mume' kwa njia isiyo halali!

    Hivyo msiwe na presha yu bukheri wa afya pika pakua kwa Mumewe wa Hiari!

    ReplyDelete
  15. ANA MIAKA 22 MTU MZIMA HUYO LABDA KAMA ANA TATIZO LA AFYA YA AKILI. ALIZOEA KUJIIBA NA MLIPO MRUHUSU TU KULALA NDIO MMEFANYA KOSA KESHANOGEWA. KESHO HAITAFIKA NA IKIFIKA ATARUDI HUKU ANALAMBA NDIMU.

    ReplyDelete
  16. Inawezekana kudhani kuwa hajapotea kafichwa kumbe kuna baya lililompata. Ulimwengu huu una mengi!

    Zena kama unaona tangazo hili ni bora ukawataarifu ndugu zako kuwatoa wasiwasi.

    ReplyDelete
  17. Yuko kwa bwana amenogewa baada ya kulala siku moja. ishallah atarudi salama, kama si yeye basi mshenga

    ReplyDelete
  18. akirudi mkampime hiv. Nadhani mabinti wa staili hii wakiwekwa ndani huwa hawana maamuzi ya kulazimisha kinga.

    ReplyDelete
  19. Inaelekea familia hizi kuna jambo mmemkosea huyu binti kwa jinsi nilivyolielewa hili tangazo.

    ReplyDelete
  20. HUYU SISTER ANAONEKANA KAJIGEMUA KULE KWETU KIGOMA TUNASEMA HIVYO,

    BADO KIJANA HUYO ANAHITAJI KUWEKWA KIDOGO AKITOSHEKA ATARUDI NYUMBANI

    ReplyDelete
  21. mzuri hivi huyu kweli kapotea ama kahama au kahamishwa???

    ReplyDelete
  22. Duh...watoto wa siku hizi SIKU ZENU ZINAHESABIKA.....yakishamshinda atarudi kisanii kwa kisingizio "eti alichukuliwa MSUKULE"......kaaz kwel kwel!

    ReplyDelete
  23. Poleni sana Wazazi na wana ndugu kwa fedheha mliyofanyiwa.

    Bi. Zenna Inshallah inawezekana yu bukheri wa afya kwa Mumewe mtarajiwa!

    La muhimu, ni dalili suala lipo nje ya taratibu za kuyafikia mahusiano halali ya Mke na Mume,,,hala hala fanyeni haraka muwatimizie taratibu sahihi zikamilike Msela asije mjaza mimba mwanenu nje ya ndoa!

    ReplyDelete
  24. Yu buheri wa afya na bwanake wanakula asali kwa maziwa!

    Mmemchelewesha Binti ilitakiwa mumpe nafasi aende kwa Mumewe tokea kitambo tu, kosa lenu hamku mchunguza mwenendo wake,

    Inaokenana alisha choka MAISHA YA NYUMBANI na sasa ameona amekua na alazimishe mwenyewe kuyaelekea MAISHA YA UNYUMBA!

    ReplyDelete
  25. Hapa ndio kinafika kipindi Baiolojia ya Maumbile na Kujitambua inapo zungumza!

    Wajameni, kipindi hiki ukiwa na ulezi au uzazi wa watoto wa Kike pia wa Kiume,,,inabidi uwe makini sana, na busara na utulivu wa hali ya juu,,,(utagombana sana),,,Asalaleee jazba, hasira na ghadhabu zinaweza kukufikisha Polisi,Jela hadi Mahakamani!

    ReplyDelete
  26. Huyo Galacha au Kachala ,Msela aliyemweka Binti mafichoni, kama ni Chinga atasimamisha safari za Misele Kiwanjani sasa anashinda Nyumbani, kama ni Mwajiriwa atadanganya kuumwa au ataomba mapumziko mafupi anashinda nyumbani!


    Galacha ,Kachala au Msela ana kandamiza, anashinda na Msuli au Taulo kiuonini, yupo chumbani ndani ya 'mabunduki' kwa kwenda mbele!!!!

    ReplyDelete
  27. inaonyesha Msela alishaanza kumbemenda Zenna muda mrefu tu! ila wazazi na ndugu wa Binti hawakujua hilo.

    Safari hii alipokwenda kwa Msela ilikuwa wamalize saa 12 jioni, wakanogewa mara 0hhh ikafika saa 2 usiku, ohhh mara saa 3 usiku,,,ohhh mara saa 4 usiku, Msela akamshawishi binti apige simu nyumbani adanganye ili walale wote,,,wakawa wamenogewa!!!

    ReplyDelete
  28. Huyu wala hajapotea ni shauri ya nondo tu.

    ReplyDelete
  29. Jamani hii ni dunia ya siku hizi naomba tusiwe na wazo moja tu la kusema kapata mume.Yawezekana kweli kapata matatizo,pamoja taarifa imetolewa Polisi lakini huenda Polisi bado hawajajua au hawaja pata uhakika wa wapi yupo huyu binti.

    Poleni wazazi wenzangu,endeleeni kufanya juhudi msizubaishwe na maneno ya watu.Hata kama yupo kwa mwanaume ndo hamjui eti!Hivyo hamwezi kubweteka.Shida yenu kubwa ni kujua mtoto yu salama kabla ya kuja ya mume.Kama kweli yu kwa mume basi hata huyo mume ni mjinga.

    ReplyDelete
  30. Ashaolewa huyo... subirini atarudi na mjukuu!!!

    ReplyDelete
  31. Wala msihangaike!

    Kama muelekeo wenyewe ni Mbagala, fanyeni kama mnasitukiza nendeni mtamkuta Msela kampakata miguuni Zenna wanakula bata kwa mrija 'wanasasambua maisha mapya matamu' pale Kiota kipya cha maraha DAR LIVE...!

    ReplyDelete
  32. Duhh bibie ameyashitukia maisha matamu ya unyumba!

    ReplyDelete
  33. Zenna amekwisha onja tamu ya asali,,,akiwa angali mdogo hajui kuwa asali hiyo huwa inageuka kuwa chungu kama shubiri!

    ReplyDelete
  34. Kudadadadeki,

    Msela atakuwa anashinda mchana kutwa usiku kucha na bukta au pensi anababua!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...