Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na wawakilishi wa kundi moja la wachuuzi (machinga) wa jijini Mwanza ambao leo January 6, 2012 walikwenda Ikulu ndogo ya jiji hilo na kumweleza changamoto zinazowakabiri, ikiwa ni pamoja na ukosefu wa mitaji pamoja na taaluma ya kufanyia biashara. Rais Kikwete ametoa milioni 10 kwa ajili yawamachinga hao kukopeshana mitaji.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na mkewe mama Salma Kikwete wakimjulia hali Mkuu wa Majeshi Mstaafu Jenerali (mst) Ernest Mwita Kyaro jijini Mwanza asubuhi ya leo Jauary 6, 2012. Jenerali mstaafu Kyaro, ambaye alikuwa mkuu wa majeshi katika serikali ya awamu ya pili, amefurahi na kumshukuru sana Rais Kikwete na mkewe kwa kutembelea.PICHA NA IKULU.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 11 mpaka sasa

  1. Yaani kutoa hiyo milioni 10 ilipaswa iwe habari ya mwisho kabisa, la msingi ni mikakati ya dhati ya kuwasaidia...si kila mtu anahitaji mkopo, na kwa hali halisi nchini, mikopo kwa masikini ni sawa na nusu ya kifo au kifo haswa. Achilia mbali wanene watakaozitolea macho hizo pesa,huwa hawajali ni kiasi gani.

    ReplyDelete
  2. We anon huna dogo kila kitu cha rais wetu mpendwa wewe ni kukandia tu. m.....vi yako!

    ReplyDelete
  3. Nakubaliana na anon. wa kwanza. Classic examples are set by India na Sri Lanka ambako masikini walivutiwa na mikopo midogo midogo na sasa wanajiua balaa kwa kushindwa kulipa na kubanwa na asasi za mikopo. Mikopo sio suluhisho BORA wakati wote, there are most basic things to cater for in order to foster long-term and unburdened development initiatives.

    Anon. wa pili, wewe ndio wale wale wa kusifia tu bila kufikiria manufaa ya muda mrefu kwa taifa. "Akisema wewe piga makofi tu, ndio kazi yako."

    ReplyDelete
  4. Wewe anon. wa pili, asante kwa kunitukana, naamini matusi yana msaada kwako. Sikuwa na nia ya kumkera wala kumkashifu mtu bali kuchangia fikra tu. Nisamehe kama nimekukera.

    ReplyDelete
  5. anony wa kwanza ni kweli tunahitaji sera madhubuti pamoja na utekelezaji. Vinginevyo wale ambao hawatabahatika kuonana na rais yaani 99.9% ya wahitaji, hawatafaidika.

    ReplyDelete
  6. to ma side i think,before give out the money or make the statement,firstly do that people have interpreur skills inorder when you give them dollar they paid back thousand grand,if they don't,make a competition to determine what they are though,and then you determine thing black and white,you give out cash or wasoever,still you have clue 4 their problem.

    ReplyDelete
  7. mchaka mchaka wa kila asubuhi saa kumi na moja na nusu

    ReplyDelete
  8. godfrey umeweka comment yako kwa inglish mbovu.. hatujakuelewa. Nyie ma anon mnaokandia mna roho za wivu tu.. u dont appreciate what u have! big up JK usisikilize negative minds...

    ReplyDelete
  9. Jamaa ni kati ya wafanyakazi wa umma waaminifu

    ReplyDelete
  10. Hapo ni nyumbani kwa Mkuu wa Majeshi mstaafu au ni Hospitali??

    Sisi tunampenda lakini Mungu anampenda zaidi huyu Mzee wetu!!!!

    Makanyaga, New York

    ReplyDelete
  11. We anon wa pili unayajua matusi au unayasikia; mbona jamaa amekujuza vizuri tu nyie ndo wale wale msiotaka kukosolewa mnapokosea; jamaa amekuelimisha vizuri sana.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...