Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa shambani kwake Msoga, Wilaya ya Bagamoyo, Mkoa wa Pwani. Shamba hilo ni la manyasi ya kulishia mifugo kwa njia ya kisasa (zero grazing), akiwa ni mmoja wa wafugaji kijijini hapo. Rais Kikwete, ambaye aghalabu hutumia muda wake wa likizo shambani kwake, pia analima pia mananasi ambayo hustawi vizuri katika wilaya hiyo. Kushoto kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mh Mwantumu Mahiza. PICHA NA IKULU

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 6 mpaka sasa

  1. Tehe Tehe hehe hehe! Ndio Mzee! :D

    ReplyDelete
  2. Hongera Mheshimiwa Rais Kikwete maana vijana wengi wa Kitanzania wanadhani kuwa kazi ni kufunga tai na kukaa ofisini, tunahitaji vijana kuwa wakulima wa kisasa ili Supermarket zijae bidhaa za Tanzania maana itafika wakati tunapata maziwa fresh kutoka South Africa.

    ReplyDelete
  3. umekuwa mfano mzuri muhwshimiwa rais,tunahtaj marais wanaowekeza ktk nchi zao ili kutoa fursa za ajira zaid na kukuza mitaji.

    ReplyDelete
  4. Kizungu wanaita HAY haya manyasi -- yanauzika sana hapa Marekani mpaka hayo manyasi yanasafirishwa toka hata Canada na huu ukame uloikumba marekani ya kusini (Texas hasa -- roli moja lilojaa manyasi kama haya la futi 53 likitolewa Southern California mpaka katikati ya Texas (mwendo wa siku mbili - kilometa kama 2000 hivi) gharama yake inakuwa around $8,000 manyasi na usafiri ndani. Sijui bei hapo home zikoje kwa wenye idea jamani?

    ReplyDelete
  5. Safi sana!! Tunajua kufuga kafundishwa na rafiki yake Lowasa lakini je hilo shamba lina ekari ngapi? Usikute shamba lenyewe eka tatu tu (Mtu wa Pwani huyo) kwao kulima ni adhabu kuu, teh teh

    ReplyDelete
  6. Hongera Mhe. Raisi JK kutuhamisisha Kilimo Kwanza halafu wewe mwenyewe ukaonyesha kwa Vitendo!

    Ni dalili njema pia Wakuu watatu wa Afrika ya Mashariki kushiriki Ufugaji wa ng'ombe,

    -Raisi Jakaya M.Kikwete:TANZANIA
    -Raisi Yoweri K.Museveni:UGANDA
    -Raisi Paul Kagame:RWANDA

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...