Uongozi wa Jumuiya ya Watanzania Rome, unayofuraha kuwajulisha wanajumuiya wake wote kuwa siku ya jumamosi tarehe 25 februari 2012 kuanzia saa nane mchana, kutakuwa na mkutano utakaoambatana na uchaguzi wa viongozi wapya wa Jumuiya ya Watanzania Rome.

Mkutano huu utafanyika kwenye ukumbi wa Ubalozi wa Tanzania Italy, mjini Rome kwenye mtaa wa Via Cortina d'anpezzo 185. 

Wanajumuiya hai wote mnaombwa muwasiliane na katibu ndugu Andrew Chole Mhella ili muweze kupata utaratibu nzima wa mkutano. Mnaweza kumpata katibu kwa e-mail hii watanzaniaroma@yahoo.it au kwa simu namba 3479094800. 

Kwa wale ambao wanapenda kuwasilisha majina yao kwaajiri ya kugombea nafasi hizi mnaombwa mtume majina yenu yakiambatanishwa na nafasi ambayo mnataka kugombea kupitia e-mail ya jumuiya hapo juu. Nafasi ni hizi MWENYEKITI, MWENYEKITI MSAIDIZI, KATIBU, KATIBU MSAIDIZI, MWEHA HAZINA NA NAFASI MBILI ZA WAJUMBE.

Uchaguzi utaendeshwa kwa kufuata kanuni za katiba.

Kwa maelezo zaidi temebeleeni hapa www.watanzania-roma.blogspot.com.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...