Naibu Katibu Mkuu Ikulu Susan Mlawi akihutubia jana jijini Dar es salaam wakati wa halfa fupi ya kumuaga aliyekuwa Mratibu wa Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za WanyongeTanzania(MKURABITA)  Mhandisi Ladislaus Lema baada kustaafu rasmi Desemba 2011
Mratibu wa  MKURABITA akitoa neno la utangulizi  jana  jijini Dar es salaam wakati wa halfa fupi ya kumuaga aliyekuwa Mratibu wa Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za WanyongeTanzania(MKURABITA) Mhandisi Ladislaus Lema baada kustaafu
Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi ya MKURABITA  na Spika wa Bunge la Tanzania Anne Makinda akihutubia jana jijini Dar es salaam wakati wa halfa fupi ya kumuaga aliyekuwa Mratibu wa Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za WanyongeTanzania(MKURABITA)  Mhandisi Ladislaus Lema baada kustaafu rasmi Desemba 2011.

 Mratibu wa Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za WanyongeTanzania(MKURABITA) Mstaafau Mhandisi Ladislaus Lema akitoa neno la shukurani jana jijini Dare s salaam wakati wa halfa fupi ya kumuaga baada kustaafu rasmi Desemba 2011 wakati wa sherehe fupi iliyoandaliwa na Ofisi ya MKURABITA.
 Baadhi ya wafanyakazi Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za wanyongeTanzania(MKURABITA)  wakitoa zawadi ya Komputya jana jijini Dar es salaam kwa aliyekuwa Mratibu wa MKURATIBA  Mhandisi Ladislaus Lema baada kustaafu 
Picha ya pamoja baada ya hafla. Picha zote na Tiganya Vincent, Dar es salaam

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 17 mpaka sasa

  1. Jina sahihi la Mratibu Mstaafu ni Mhandisi Ladislaus SALEMA na sio Lema.

    Mdau Tallinn.

    ReplyDelete
  2. Mstaafu Mzee Salema karibu Maskani Mtaani tulisukume gurudumu la maendeleo!

    Ingawa utakuwa tayari wame kucheki kidogo na umejipanga mwenyewe kwa upande wako,,,Huku Mtaani ndio utaushuhudia 'MKURABITA' wenyewe kiukweli ulivyo kwa vitendo kuliko ulivyokuwa unapokea Makabrasha ya makaratasi ya Tafiti na Tarifa kwa njia ya simu ukiwa MEZANI OFISINI!

    ReplyDelete
  3. Mhe. Mstaafu Laslaus Salema, huku Mtaani ndio ilipo Maabara kamili ya 'Mkurabita' yaani matekelezo kwa vitendo kwa hali halisi kuliko Ofisini ulipokuwepo.

    Kama utaitumia nafasi hii utaweza andika vitabu na kuandaa Tafiti zenye Uhalisia kuliko theory uliyokuwa ukiifanya kabla!

    ReplyDelete
  4. Mtaani kuna ACTUAL iliyo 'PRACTICAL' halisi ya huo Mkurabita kuliko PAPER WORK ya 'THEORY' iliyobaki Ofisini kwako nyuma!

    ReplyDelete
  5. Mtaani kuna ACTUAL iliyo 'PRACTICAL' halisi ya huo Mkurabita kuliko PAPER WORK ya 'THEORY' iliyobaki Ofisini kwako nyuma!

    ReplyDelete
  6. Mkurabita kabla ya Kustaafu ni Mpole kama Samaki Dolphin 'Pomboo' lakini baada ya Kustaafu Mkurabita anakuwa Mkali sana na meno makali kama Mamba!

    ReplyDelete
  7. Mkurabita muutambue Machango wa Mzee Salema muwe mnamtafuta kwa Ushauri kama ikibidi yanapokuwa mambo magumu 'Ukubwa ni Jiwe' au 'Jungu Kuu halikosi ukoko' awamegee uzoefu wake kwa faida ya wote,,,pia mjenge Utamaduni wa Kumwalika ktk ghafla mbalimbali Ofisini!

    ReplyDelete
  8. Picha ya Chini kabisa walipokuwa wamekaa Mstaafu akiwa katikati anatweta anakuwa kama haamini vile kuwa Kungele imelia na sasa anag'atuka!.

    Kwa 'Msala' na 'Libeneke' la Ugumu wa Maisha uliopo sasa, inaonekana wengi hawako na ridhaa ya kuondoka kazini,,,nadhani BORA tufanye ILI MRADI UNAFANYA KAZI VIZURI hakuna kustaafu hadi KIFO KIKUKUTE OFISINI!

    ReplyDelete
  9. Bahasha za Mezani kwa Mzee ndio zimefikia kikomo,,,kilichobaki ni Fedha ulizonazo Mkononi unakuwa Mr. CASH!

    ReplyDelete
  10. Weweee Mzee wa Kichagga huyu ameshajiandaa!

    A ngekuwa mtu wa Mwambao hatihati tungekaa mkao wa Msaada wa Imani!

    ReplyDelete
  11. Wakati mwingine ni bora kuwa huru Ukafanya mambo yako baadabya Kustaafu kuliko taharuki na lawama ya kazi za Mamlaka ktk Utumishi wa Ajira kwa kujieleza na kuandika Taarifa hasa mambo yanapokwenda kombo.

    ReplyDelete
  12. Mhe. Mstaafu 'Mkurabita' ule kabla ya Kustaafu ukiwa Ofisini ulikiuwa ni PAPER TIGER yaani 'Chui wa Karatasi' na sasa Baba unalekea ukabiliana na 'Mkurabita' wa 'Chui mwenye nyama na Damu'!

    ReplyDelete
  13. Andaa Bustani ya Mchicha na Matembele ktk uchochoro wa nyumba, imarisha banda la kuku uani na Banda la ng'ombe uani!

    Tafuta Mmasai makini umkabidhi zizi la mifugo yako hiyo ndio ajira yako baada ya Kustaafu.

    ReplyDelete
  14. What is Mkurubita? Dont lough at me

    ReplyDelete
  15. Suala la Kustaafu:

    Kwa nchi zetu hizi ambazo mambo ya uchumi yapo ktk Mtindio Siku ya Kustaafu ni kama Siku ya Kufa au Siku ya Kuzamishwa Kaburini!

    KIZA KIMETANDA NA MAISHA YANAFIKIA UKINGONI

    ReplyDelete
  16. Inaonekana Mzee alipendelea aendelee na kazi, lakini Sheria ya Utumishi wa Umma ndio inamzuia!

    ReplyDelete
  17. Mnhhh,

    Hapo ktk picha ya chini Mzee amestuka kuwa sasa anakoelekea siko kabisa, matumaini yanaanguka!

    BUNDI WA KUCHACHA ANAUNGURUMA!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...