Katibu wa Itikadi na Uenezi wa
CCM Bw. Nape Nnauye ametangaza majina ya waliopendeekzwa na halmashauri kuu
kuwa wagombea viti wa chama hicho katika
bunge la Afrika Mashariki.
Kwa Tanzania Bara wanawake
waliopendekezwa ni 12 wanaume 17 wakati kwa Zanzibar wanawake waliopendekezwa
ni watano na wanaume wanane.
Nape alisema vigezo vilivyotumika viko ndani ya
chama hicho na kwamba chama kinajivunia kujitokeza kwa wasomi wengi kuwania
nafasi hiyo wakiwemo vijana na akinamama.
Aidha, alisema Kamati Kuu imeteua wajumbe watatu
wa kusimamia uchaguzi huo ambao ni
Abdulrahman Kinana, yeye mwenyewe Nape na Dogo
Mabrouk.
Alitaja wanawake waliopendekezwa kwa Tanzania Bara
kuwa ni Janeth Mmari, Janet Mbene, Fancy Nkuhi, Nora Mukami, Shally Raymond,
Shy-Rose Bhanji, Ngollo Malenya, Godbertha Kinyondo, Hamidah Kalua, Angela
Kizigha, Happiness Lugiko na Ruth Msafiri.
Kwa upande wa wanaume Bara aliwataja Dk. Aman
Kabourou, John Ngongolo, Dk. Evans
Rweikiza, Siraju Kaboyonga, Benard Murunya, Dk.
Edmond Mndolwa, Christopher Awinia na
Dk. Hilderbrand Shayo.
Wengine ni Makongoro Nyerere, Adam Kimbisa,
Elibariki Kingu, Simon Berege, Mrisho Gambo, Handley Mafwenga, William
Malecela, Mussa Mnyeti na Godfrey Mosha.
Wanawake waliopendekezwa upande wa Zanzibar ni
Septuu Mohammed Nassor, Safia Ali Rijaal, Rukia Seif Msellem, Sabah Saleh Ali
na Maryam Ussi Yahya.
Wanaume Zanzibar kwa mujibu wa Nape ni Dk. Said
Gharib Bilal, Abdallah Ali Mwinyi, Dk. Haji
Mwita Haji, Dk. Ahmada Hamad Khatib, Zubeir Ali
Maulid, Khamis Jabir Makame, Abdul-Aziz Salim na Mbwana Yahya Mwinyi.
Bunge hilo kwa sasa lina wajumbe 52, wakiwa tisa
kutoka kila nchi mwanachama wa EAC
pamoja na wajumbe wengine saba wanaoingia kwa
nafasi zao.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...