Ankal na mdau John  Ulanga wa The Foundation for Civil Society (BOFYA HAPA) wakiwa na Rais Mstaafu wa Nigeria Jenerali Olesegun Obasanjo uwanja wa ndege wa Sao Paulo nchini Brazil leo. Jenerali Obasanjo, aliyekuwa anatoka Brazil kuelekea Afrika Kusini, alishangaza wengi kwa kuja kukaa na akina ankal kwenye sehemu ya kusubiria safari kwa abiria wa 'ecocomy class' badala ya kwenda kungojea muda wa safari katika Lounge kama ilivyo kawaida kwa wasafiri wenye tiketi za daraja la kwanza. Isitoshe alikula stori na Ankal na John kwa namna ambayo haikuwa rahisi kumaizi kuwa huyu ni mkuu wa nchi mstaafu. Ila aliapotua jijini Johannesburg tu, Jenerali Obasanjo hakuwa mwenzao tena, maana maafisa ubalozi na wana usalama wa Sauzi walimzingira na kumpeleka VIP chapchap....

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 14 mpaka sasa

  1. Safi sana Ankal! Kumbukumbu nzuri hiyo :)

    Hope you had a good time bro.

    Mdau
    Buckinghamshire

    ReplyDelete
  2. naona hata mobile phone ana ya mchina

    ReplyDelete
  3. True leader and gentleman,mtu wa watu kweli.

    ReplyDelete
  4. Nimeipenda FULANAZZZZ! AKAL nitahakikisha unainadi na nitainunua . Taswira makini hii

    ReplyDelete
  5. Hizo nguo alizovaa ni nguo za kulala au????

    ReplyDelete
  6. Ankal hako kafulana ka mistari mistari tena msalie mtume basi nipe mimi angalau nipate mavumba ya jenerali obasanjo umekashika kafulana hako muda mrefu sasa au kana dawa ya babu wa kikombe unakapenda najua nitumie mimi kwa anuani hii nijaribu bahati yangu labda nitapata kuonana na pope benedict.

    mdau.

    mongolia.

    ReplyDelete
  7. jamani huko ulaya wana mambo hakuna VIP? au na nyie vile mlikuwa na JK ndo Ma VIP wenyewe?

    ReplyDelete
  8. Ankal Obasanjo kuja kukaa na ninyi ana lake jambo sio bure.

    Ktk maongezi mliyofanya naye hapo muda wote huo atakuwa amepata kitu au alikuwa anatafuta kitu!

    ReplyDelete
  9. teh!teh! Ze fulanazzzzzzzzzzzzzz!! ituwakilisha babu kubwa
    wadau FFU

    ReplyDelete
  10. Ankal the Fulanas umepewa na babu wa loliondo nini? Naona haitoki ukiwa unaenda majuu tu ipo mwilini au ndio nguzo ya kukulinda usipate balaa tetethhhetetetehh.nafikiri sasa imefika wakati tuifanyie mazishi ili tuiweke kwenye jumba la makumbusho.

    ReplyDelete
  11. watanzania kweli ni wasafiri yani wapo kila kona ya dunia na ukiangalia nchi yao haina hata vita useme wamekimbia vita

    sasa wewe mdau uliopo huko MONGOLIA kweli kiboko na ni shujaa mmmh wabongo noma.

    ReplyDelete
  12. Mr Ulanga uko juu sana kuendeleza The Foundation Civil Society, tunahitaji watendaji wa kujituma kama wewe,Hongera sana.

    ReplyDelete
  13. ze fulanazzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzz

    ReplyDelete
  14. Ankal sio bure hiyo 'fulanazzz' ni ya Tambiko!

    Jamaa walikushuhudia ulipokuwa Ujerumani miaka kadhaa ukiwa unaifua kwa mikono fulana kwa maji na sabuni bila washing and drying machine !

    Je ni kweli hiyo ni fulana ya kawaida?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...