Waziri Mkuu  Mh Mizengo Pinda akizungumza na Mbunge wa Arumeru Mashariki ,  Mh Joshua Nassari kwenye viwanja vya Bunge Mjini Dodoma
 Mbunge wa Busega, Mh Dr. Titus Kamani (mwenye kaunda suti katikati) akiwa katika picha ya pamoja na madaktari wanafunzi kutoka chuo cha Bugando, Mwanza, ambao walitembelea Bunge mjini Dodoma
Mbunge wa Busega, Mh Dr.Titus Kamani akisalimiana na madaktari wanafunzi wa Chuo cha Bugando,  Mwanza ambao Aprili 18, 2012 walitembelea Bunge Mjini Dodoma

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 6 mpaka sasa

  1. Ankoooo, pole na mihangaiko ya kutafuta ugali pamoja na kupotelewa na rafiki yako mpendwa kanumba,ila na sisi majonzi yalitukumba.LEO NAKUOMBA INIWEKEE HII KWENYE BLOGI YETU TUKUFU ILI WENZANGU NAO WACHANGIE HOJA. KWANZA NAWAULIZENI JE ? MMESOMA MICHUZI YA LEO TAREHE 19 , 2012 ANGALIENI MBUNGE WA BUSEGA AKISALIMIANA NA MADAKTARI WANAFUNZI WA MWANZA,SWALI LANGU NI FUPI SANA ,KWA NINI SIKU HIZI WATANZANIA TUMEKUWA WADOGO WADOGO SANA, JE ? MBEGU ZILE KUBWA KUBWA KAMA ZA MABABU ZETU ZIMEKWENDA WAPI ?? JAMANI HILI SWALI SIYO UTANI,IKO HAJA YA WANASAYANSI KUINGIA KAZINI KUFANYA UTAFITI,TAIFA LISIJE LIKAWA LA WATU WA MRABA MMOJA BADALA YA KUWA JITU LA MIRABA MINNE-HODARI NA AFYA ISIYOTISHWA NA KADUDU KADOGO KAMA MBU. ZAMANI HUKO MWANZA WALIKUWA WANAZALIWA WATOTO WA NGUVU AU KWA KISWAHILI CHA MWANZA (JILI TOTO) SIYO KATOTO.SASA JAMANI HIZI MBEGU NDOGO NDOGO ZIMETOKA WAPI ?? AU LISHE IMEKUWA NDOGO SIKU HIZI ??? NI MIMI ZEBEDAYO WA ZEBEDAYO (MWANZA)

    ReplyDelete
  2. Vijana njaa tupu hamushibi ndiyo maana hamukui kisawasawa.

    Halafu hiyo mbegu kubwa uwe mrefu mnene huwezi kutosha kwenye Hiace au Noah, itabidi uwe unatembea kwa miguu kila siku.

    ReplyDelete
  3. Naomba kuuliza: nguo aliovaa Mh. Nassari ni Kaunda suit? naona kama ina Chinese collar. Naomba nielimishwe.

    ReplyDelete
  4. nimependa sana picha ya waziri mkuu na mbunge nassari wa arumeru, huyu nasari atakuja kuwa waziri one day. Natabiri

    ReplyDelete
  5. Kwani hao madaktari wote wamezaliwa Mwanza??Usitake kutuchanganya nawe....Halafu hao madaktari wanafahamu madhara ya miili mikubwa unayoisema..so hao unaowaona hapo wanaitawala miili yao.Unapenda Kitambi na mafuta hey??

    David V

    ReplyDelete
  6. Ndugu Zebedayo, pole kwa kutojua, wazee wetu walikuwa hawavunji amri ya sita kama sasa, sasa hivi amri ya sita kila mahali hadi kufanya unapomtafuta mtoto anakuwadhaifu/weak maana mizizi ilikuwa imechoka

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...