ILE meli maarufu kama 'Meli ya Magufuli' ambayo Serikali ya Tanzania iiliansa katika Eneo lake la bahari ya Hindi ikivua samaki bila ya kibali imenza kuzama baharini na imeharibika vibaya. 


 Inaelezwa kuwa Meli hiyo ya Tawaliq 1 Machi 8, 2009 ilikamatwa ikiwa na tani 293 za samaki aina ya Jodari iliyowavua katika bahari ya Hindi ndani ya Ukanda wa Kiuchumi wa Tanzania (EEZ), bila kuwa na kibali. Meli ya Tawaliq 1 ilikamatwa ikiwa na wavuvi 34 na hadi kufikia tamati ya kesi hiyo jumla ya wavuvi 20 walitiwa hatiani. 


 Lakini licha ya Mahakama kuamuru meli hiyo itaifishwe kwa sababu ilikuwa haijulikani na tume inayojihusisha na shughuli za uvuvi katika Bahari ya India (IOCT) lakini meli hiyo imeanza kuzama kama inavyoonekana pichani. Kuzama kwa meli hiyo ni kutokana na kutoboka baadhi ya maeneo hivyo kuingiza maji ndani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 10 mpaka sasa

  1. KUSEMA KWELI TANZANIA TUNA TIA AIBU. HILI TAIFA LINAELEKEA KUSIKO. HII MELI NI YA MAMILIONI YA DOLA INAOZESHWA KIUZEMBE. KWA NINI ISNGEKABIDHIWA TAFIRI AU MBEGANI WAKAITUMIA KWENYE TAFITI NA UVUVI? EE MUNGU TUNUSURU, EMBU WAAAMSHE HAWA VIONGOZI WETU MAANA HATA WEWE HUFURAHISHWI NA HII HALI. MUNGU TUSAMEHE MAKOSA YETU.

    ReplyDelete
  2. Wakati taasisi ya utafiti ya TAFIRI ikiwa haina hata chombo kimoja chenye hadhi ya meli hii , na wala serikali haina uwezo wa kununua kwa sasa, ninashangaa kwanini wasipewe meli hii inayoozea baharini?? KWELI SERIKALI HAMNAZO

    ReplyDelete
  3. wenzetu wakitaifisha wanatumia, sie tukitaifisha tunaharibu kama wehu......kweli aliyewalaani watanzania awaonee huruma wanataabika na hii laana.

    ReplyDelete
  4. serikali yetu inapenda kesi za kijinga ambazo matokeo yake zitaweza kuzalisha wadudu wa rushwa kuongezeka

    nina maana kusema hayo kwa mfano hao waliokamatwa kwenye meli hiyo itafika siku ya siku wataachiwa mmoja mmoja kutokana na uwezo wa utoaji rushwa

    jambo la pili ukizingatia kuwa kama samaki walishavuliwa ni vyema kuwapa hao watuhumiwa onyo kali na kuwapa masaa 24 kuiacha nchi na kukimbilia makwao

    sasa ukiangalia hapo watuhumiwa wataachiwa kwa njia ya rushwa na hapohapo watakuwa wametuachia uchafuzi wa mazingira baharini

    hilo limeli litaleta uchafuzi wa mazingira na serikali haitojuwa ni wapi pakulipeleka sasa ndugu wadau hamuoni kuwa serikali yetu inapenda kujiongezea mizigo isiyokuwa na misingi?

    ReplyDelete
  5. Tunapotoka hatupakumbuki, na tunapo elekea hatupajui.. Tanzania imekuwa shamba la bibi..

    ReplyDelete
  6. Hivi ina maana Mawaziri wote hakuna mwenye akili hata mmoja wa Kumshauri Raisi? Mbona mtu kama Membe, Nchimbi, Hussein Mwinyi, Sita wanaonekana wana busara wameshindwa kuweka kwenye AOB kwenye baraza la mawaziri?

    Sasa faida iko wapi, ni bora hiyo meli wangeachiwa hao wavamizi, maana samaki wenyewe hatuwavui, wanakufa kutokana na umri mkubwa, si bora watu wengine amabao ni wa Mungu wakafaidi kuliko hao samaki kuacha waozee baharini?

    Nilichojifunza ni kwamba, viongozi wetu sehemu yeyote ambayo haina pesa hawashughuluki nao, wote macho yao yapo TRA, NSSF, Migodi, Vitalu vya uwindaji, kutembea na bundiki kujilinda, safari (perdiem), kumalizana kisiasa, uraisi 2015, posho, marupurupu, n.k.

    Watanzania tumekwisha, hatutakaa tuendelee hata siku moja mpaka Issa ataporudi mara ya pili.

    ReplyDelete
  7. Hiyo scraper mnataka wapewe watafiti ili wazame nayo? Iache tu izame yenyewe

    ReplyDelete
  8. hiyo meli si ingeletwa kigoma ifanye kazi ziwa tanganyika? Kigoma tunaweza.. angalia jinsi MV Liemba inavyodunda ingawa ni meli ya tangu vita kuu ya 1 ya dunia.

    ReplyDelete
  9. Nasikia wameiba vitu kem kem toka kwenye hiyo meli na wakaamua kuitoboa izame kupoteza ushaidi. Niliona watu wa kigamboni wakitoa ushuhuda Mlimani TV kama sikosei. Walikuwa wakisema askari wamekuwa wakitoka na vitu mbali mbali including mafuta toka kwenye hiyo meli

    ReplyDelete
  10. Kudadadeki kweli nchi imeoza viongozi wamevimbiwa na rushwa mpaka hawajui cha kufanya bye bye ccm 2015 mageuzi daima.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...