Mkurugenzi wa Kamati ya Miss Tanzania kupitia kampuni ya Lino Ntenational Agency, Hashim Lundenga akizungumza na baadhi ya washiriki wa shindano la Redds Miss Kurasini jioni ya leo Mei 22,2012 wakati wa mazoezi yao yanayoendelea katika Ukumbi wa Equator Grill jijini Dar es Salaam. Redds Miss Kurasini imedhaminiwa na NAEEMS WAER , wauzaji wakubwa wa nguo za aina zote jijini Dar es Salaam wenye maduka yao Kariakoo na Mwenge, linataraji kufanyika Mei 25, mwaka huu ukumbini hapo.
Lundenga aliwataka warembo hao kujiheshimu maana urembo ni kazi kama zilivyo kazi nyingine na warembo wengi wanaojiheshimu na kuwa na tabia njema katika jamii huwa na mafanikio makubwa.
Kamati hiyo pia ilihudhuria na Katibu Mkuu wake Bosco Majaliwa, Mkuu wa Itifaki, Albert Makoye, Ofisa Habari, Aidan Ricco na Ofisa wake Yason Mashaka.
Warembo wakimsikiliza kwa makini Mkurugenzi wa Mashindano hayo kitaifa, Hashim Lundenga.
Warembo wanaoshiriki shindano la Redds Miss Kurasini wakiwa katika Picha ya pamoja baada ya kuzungumza na Kamati ya Miss Tanzania.
Wakati Nameems Wear wakiwa ni wadhamini wakuu, wakisaidiwa na Reds, Dodoma wine, Clouds FM, Lady Pepeta, Father Kidevu Blog, Jambo Leo, Aucland Tours & Safaris, Candy Bureau de Change, Flexip, PJ Amusement, Renzo Salon na Madishisha Video Production.
Aidha Jumla ya warembo 16 wamejitokeza kuwania taji la Redds Miss kurasini 2012, ambalo taji linashikiliwa na Top Model wa Miss Tanzania 2011, Mwajabu Juma.
Akiwataja warembo waliopo kambini na kunolewa na Mwajabu Juma akisaidiwa na Malkia wa vipaji wa Miss Tanzania 2011, Rose Hurbert ni Mariam Sadic (19), Johari Juma (20),Linda Deus (20),Irene Sostheness 20),Neemadoree Sylvery(29),Edna Magige (22), Lindanancy Joseph(20), Elizabeth Mkende (19), Betty Peter (22), Jennifer Njabili (18), Lilian Joseph (20), Farida Mrope (23),Christina Moses (20), Angle Gasper (19), Flaviana Maeda(22) na Sia Kimambo (19).


Hii picha inazungumza mengi: kamati ya Miss Tanzania yote ni wakaka na washindani wote ni wadada. Is there something am missing?
ReplyDeleteHivi Lazima hawa wamiss wawe wembamba? Miye skubaliani na hili!
ReplyDeleteHata kama mtu si kuwa mnenenee wa obesity, jamani maumbile ya waTZ wanamama si haya haaaaa hawa wamekondeanaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa
hapo lundenga unafurahi kuona vipaja vya hao wanyange kazi kweli kweli,hiki ni kipindi cha kamati ya lundenga kupata mishiko ya nguvu yetu machooooooooooooo
ReplyDeleteHebu angalia hiyo meza jinsi ilvyochoka!! Yaani.........!!! Na watu ndio hapo hapo wanafanya mkutano, ujanjaujanja tu!
ReplyDeleteHuyu Boss wa Miss Tz. amepitwa na wakati na umri umemtupa mkono aachie vijana wabunifu labda wanaweza kutufikisha mbali kimataifa! kila siku lundenga na hamna kitu.
ReplyDeleteWadhamini jitoeni kwani hakuna jipya wekezi ktk mambo ya maana na yenye maslahi kwa wengi kuliko huu upuuzi
Hivi ili kuwa mrembo lazima uache mapaja nje, jamani watanzania tuache ulimbukeni, sasa si mvue kabisa? Unaweza kuvaa nguo ya heshima bila kuacha mapaja na matiti nje na urembo wako ukaonekana
ReplyDeleteUrembo ni pamoja na mzingira mazuri Mh Lundega, hiyo meza hapo haistahili kutumiwa hata na Mama lishe wa gomapembe let alone miss whatever kambi lol.
ReplyDeleteVery interesting...!! Waandaji ote kina kaka af washindani kina dada....duuuh!!
ReplyDeleteYah that Commitee isnot gender sensitive
ReplyDeleteHakuna hat dada mmoja alyelalamika
ReplyDeleteMdau wa kwanza umesema neno. Hivi hakuna wamama wa kuendesha hay mashindani ya mabinti?
ReplyDeleteHiyo meza aliyoandaliwa Lundenga nemeipenda!!
Hiyo meza ilivyochakaa. Sijui walikosa meza safi na nzuri. Kweli bongo tambarare.
ReplyDeleteHivi wewe Lundenga kwa mavazi na mikao waliyokaa washiriki wa miss Kurasini mwanao anaweza kushiriki?
ReplyDeletehivi haya mashindano ni mpaka wavae na kukaa mikao ya hasara namna hiyo?
lundenga wewe una watoto wakike kweli,mtu mzima kabisa unawadhalilisha watoto wa wenzio kisa hela? moto unakusubiri wewe usiye na heshima wala adabu!
mvalishe na mkalishe binti yako hivyo mbele ya kadamnasi!
SHAME UPON YOU LUNDENGA!
Tell me a out it
ReplyDeleteWanawake sio matapeli
ReplyDeletena hiyo meza du!!! jamani tujitahidi hata kuweka kanga juu meza nayo safi du.
ReplyDeleteNi hayo tu ni mimi
Mr Nyamaimewahi Kunikabashingoni
Hawa viongozi wa u-miss hakuna kustaafu kweli!Toka mambo haya yameanzishwa upya Lundenga Lundenga Lundenga tu.Hii ndo nini jamani.
ReplyDeleteNasehemu zingine hivi hivi watu huzeeka na nyadhifa.Hivi ndo utaratibu gani huu.
Tulitoka enzi za kina Kubaga,Masauni,Bayi,sasa Tenga Tenga Tenga.Hapa kweli turakuwa tunapata mabadiliko katika mambo yetu!
Mnhhh !!!
ReplyDeleteHiyo meza aliyokaribishwa Bwana Mkubwa Lundenga ni kama vile meza ya kukatia supu au kuwekea mabakuli ya supu ya utumbo!
Ahhh Lundenga ni Mkubwa wenu inabidi mumpe nafasi yake ,kulikoni? vipi Waandaaji Miss Kurasini ???
ATI NI KWELI NI LAZIMA AONJE?
ReplyDelete