Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Kim Poulsen leo (Mei 14 mwaka huu) ametangaza kikosi cha wachezaji 25 kwa ajili ya mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia hatua ya makundi Kanda ya Afrika dhidi ya Ivory Coast.
Akitangaza kikosi hicho ambacho kitaingia kambini kesho kutwa (Mei 16 mwaka huu, Kim amesema uteuzi wake umezingatia uwezo wa mchezaji uwanjani, nafasi anayocheza na ubora wake.
Wachezaji walioitwa ni makipa; Juma Kaseja (Simba), Mwadini Ally (Azam) na Deogratius Munishi (Mtibwa Sugar). Mabeki ni Nassor Masoud Cholo (Simba), Aggrey Morris (Azam), Amir Maftah (Simba), Erasto Nyoni (Azam), Kelvin Yondani (Simba), Waziri Salum (Azam), Shomari Kapombe (Simba) na Juma Nyoso (Simba).
Viungo ni Mwinyi Kazimoto (Simba), Salum Abubakar (Azam), Nurdin Bakari (Yanga), Jonas Mkude (Simba), Shabani Nditi (Mtibwa Sugar), Edward Christopher (Simba- U20), Mrisho Ngasa (Azam) na Frank Domayo (JKT Ruvu- U20).
Washambuliaji ni Mbwana Samata (TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo), Ramadhan Singano (Simba-U20), Simon Msuva (Moro United- U20), Thomas Ulimwengu (TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo), Haruna Moshi (Simba) na John Bocco (Azam).
Stars inayodhaminiwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia bia ya Kilimanjaro itacheza mechi ya kirafiki nyumbani Mei 26 mwaka huu dhidi ya Malawi kabla kuivaa Ivory Coast ugenini Juni 2 mwaka huu jijini Abidjan.
Ningeshauri tutumie wachezaji wa under 23 ili baada ya miaka miwili hivi wawe wameiva. Tunaweza kuongeza wakubwa kama watatu tu wa kuleta changamoto na uzoefu.
ReplyDeleteDu, naona wachezaji wa yanga wanaendelea kula jeuri ya kumpiga refa. Kikosi kizima ameteuliwa mmoja tu.
ReplyDeleteHamna kitu..Hawa karibu 90% walishashindwa..jaribuni 'fresh legs'.Kuna mdau mmoja kwenye hii blog ya jamii alichangia sikumbuki ni mawaziri wa juzi au..anyway,aliongelea kutoa chungwa kwenye kikapu na kuweka ndimu.
ReplyDeleteDavid V
Yanga mmoja tu, sawa tutakutana taifa
ReplyDeleteHii si timu ya kuifunga Ivory Coast.
ReplyDeleteMmmmh hii kali yaani kufugwa 5 ndo imekuwa hatujui mpira nini? je uamuzi wa kocha mkuu ndo wa mwisho? YANGA OYEEEEE!
ReplyDeleteHii ni Simba SC. au Taifa Stars, huyu kocha atakuwa katumwa!
ReplyDeleteAmini Amini nawaambia, huyu kaanza vibaya na sababu mnaijua. Kama hamtaniamini subirini hatima yake.
ReplyDeletePole Kim, busara ndogo imekuponza.
Huyo ni kocha wa timu ya Taifa au ni Kocha wa timu ya Simba?
ReplyDelete