Baadhi ya wachezaji wa Simba wakiwa na huzuni baada ya timu yao kutolewa kwa mikwaju ya penati na Al Ahly Shandy katika mchezo wa marudiano huko Sudan. Katika mchezo wa kwanza uliofanyika wiki mbili zilizopita jijini Dar es salaam Simba ilishinda magoli 3-0 na kujiweka katika nafasi nzuri ili kusonga mbele katika michuano hiyo ya Kombe la Shirikisho inayoandaliwa na Shirikisho la vyama vya mpira wa miguu Afrka (CAF) kabla ya kulinda ushindi wake mnono ilioupata jijini Dar es salaam kwa  kukubali kipigo hicho kilichowasukumiza nje ya mashindano hayo.  Al Ahly ilipata penati zote tano baada ya kushinda bao 3-0, na Simba walikosa penati mbili. Picha na Shafii Dauda






Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 17 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 14, 2012

    Shandy walikosa penalty moja na simba wakakosa mbili kupitia kwa Mafisango na Kaseja. Wachezaji wote walipiga akabakia Kaseja ambaye alikosa ya mwisho.

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 14, 2012

    AL AHLY SHANDY:

    Mwarabu kwa fitina na mipango si mchezo!

    Angelieni sisi tumewakaribisha Waarabu kwa ukarimu na huduma kede kede, lakini sisi tunafika kwao wanatuhenyesha, Hoteli nje ya mji, wanatulisha Biriani ya nyama ya ngamia iliyopikwa na mafuta kibao, matokeo yake Mhe. Mbunge ambaye ndio Mwenyekiti na Raisi wa Timu ya Msimbazi anaharisha kupita kiasi hadi anashindwa kufanya 'mipango yake' inayojulikana ili kuiokoa timu!

    Mwarabu kwa fitina na mipango mchezo?

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 14, 2012

    Mimi ni Liverpool na Yanga, jana usingizi mnono kabisa....

    ReplyDelete
  4. AnonymousMay 14, 2012

    Afadhali looooooo! Tutapumua mjini hapa

    ReplyDelete
  5. AnonymousMay 14, 2012

    Jee waarabu walibebwa na refa?

    ReplyDelete
  6. AnonymousMay 14, 2012

    HAHAHAHAH........NDIO MATATIZO YA KUTANGULIA NA BAISKELI YA MITI....HOME CAMING....KELELE NYINGIII MPAKA BUNGENI NA NINI....KWISHNEEEEE

    ReplyDelete
  7. AnonymousMay 14, 2012

    Hujuma za waarabu wa Sudan zisinyamaziwe.

    Hivi kwa nini tusigomee kucheza na waarabu mpaka michezo ichezwe kwenye neutral ground?

    Toka Simba wamefika sudan ni hujuma mtindo mmoja!

    ReplyDelete
  8. AnonymousMay 14, 2012

    Ankal
    Hiyo ni bahati mbaya juhudi zilionekana isipokuwa makosa madogo yameigharimu timu. Tujifunze kwa yote tuliyoyapitia ili mwakani tusiishie hatua hii. Hongereni msikate tamaa.
    Big up SSC.

    ReplyDelete
  9. AnonymousMay 14, 2012

    hii ni kweli???
    Simba damu Ottawa

    ReplyDelete
  10. AnonymousMay 14, 2012

    Haya, karibuni nyumbani watani tuendeleze tunayoyaweza...hayo mengine tuwaachie wenyewe maana tumeshawasindikiza vya kutosha.

    ReplyDelete
  11. AnonymousMay 14, 2012

    Wachezaji wamechoka. Halafu mtapelekaje timu Sudan kabla ya kutanguliza mtu wa kutayarisha makazi na usafiri wa kutoa airport had hotelini hadi huko shendy? Kipa wa Ferrovierio ya Maputo aliwatahadharisha, mkamwona yeye ni wa kuja leo karudi kesho!

    ReplyDelete
  12. AnonymousMay 14, 2012

    Bora wametolewa sasa tunalala tumetukanwa sana wiki hizi mbili mpaka tukawa tunashindwa hata kutembea, lakini sasa hivi afadhali na jana tumepata usingizi japo kidogo, kelele zimepungua. Simba oyeeeeeee!

    ReplyDelete
  13. AnonymousMay 14, 2012

    SAFI SANA KELELE ZILIKUWA NI NYINGI SANA KARIBUNI NYUMBANI MSIMBAZI TUENDELEZE UCHAWI WETU WA KULOGANA KWENYE SOKA NIMEPOKEA HII TAARIFA KWA FURAHA KUBWA SANA.

    ReplyDelete
  14. AnonymousMay 15, 2012

    Tatizo hapa ni mechi ya yanga. Yanga waliwaachia na wao wakaona wanajua mpira kuliko yanga. Thubutu. Wakasema kwa kuwa tumemfunga yanga basi timu yoyote Africa tutaifunga.

    ReplyDelete
  15. AnonymousMay 15, 2012

    simba luala

    ReplyDelete
  16. AnonymousMay 15, 2012

    Ahhh Mwarabu ndio unawaweka Wachezaji wetu chumba cha makabati wazi Hotelini au Uwanja wa Ndege?

    Jamani Waarabu wakija safari nyingine na sisi tuwaweke hukooo kando ya mji na tuwalishe 'dona' na 'dagaa' wachungu!

    ReplyDelete
  17. AnonymousMay 15, 2012

    Simba amefyata mkia,,,umezama hadi uvunguni mwa tumbo lake!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...