Na Woinde shizza,Arusha

Dini ya hindu kupitia dhebhebu la shri swaminaraya imeahidi kutoa elimu kwa waumini wake pamoja wananchi wasio wahumini kuhusiana na sensa ya watu na makazi ambayo inatarajiwa kufanyika mapema mwezi agosti.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini arussha leo,Ofisa Uhusiano wa dhehebu hilo Kaushik Vasan alisema kuwa dini yao ipo tayari kutoa ushauri kwa waumini wao pamoja na wananchi kwa ujumla ili kuweza kubaini nini maana ya sensa ambapo pia watawahamasisha wananchi hao kushiriki zoezi hilo siku hiyo.

Alisema kuwa pia kwa kutumia sherehe za uzinduzi wa jengo la msikiti wao ambao wameujenga jijini hapa ambao wanatarajia kuzindua leo watahamasisha watu wote ambao watahudhulia sherehe hizo kushiriki zoezi hilo.

Vasan alisea kuwa kutokana na umuhimu wa sensa hiyo ya watu na makazi wataisaida serikali katika kuhamasisha waumini wake na wakazi wa jiji hili kwa ujumla juu ya umuhimu wa kujiandikisha wakati wa sensa.

Akiongelea uzinduzi wa msikiti huo alisema kuwa mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Ghanshyam Charan Swami ambaye ni mmoja wa wasaidizi wa kiongozi wao,mkuu wa dini hiyo ambaye ni HDH,Pramukh Swami Maharaj (91) aishiye nchini India.

Alibainisha kuwa katika uzinduzi huo wanatarajia zaidi ya wageni 800 kutoka nje ya nchi ambao watafika kusherekea pamoja zoezi hilo ,huku akibainisha kuwa mbali na masuala ya kiimani  wanajikita pia katika kusaidia jamii ikiwepo kupanda miti kwa ajili ya mazingira ,kutoa huduma mbalimbali za kijamii kama vile kusaidia hospitali mbalimbali vifaa ,pamoja na kuwasomesha watoto yatima na wale ambao wanaishi katika mazingira hatarishi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 23, 2012

    Kwani huwa wahindi hawashiriki sensa? Kama ndivyo wanastahili kuchukuliwa hatua. Hawawezi kujiamulia mambo wakati wako kwenye nchi inayoongozwa kwa mujibu wa sheria.

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 23, 2012

    That is not true.
    We all have been participating katika sensa.
    We are citizens of this great nation and all rules & the law are applicable to us like they would be applicable to others...Mungu Ibarike Tanzania

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...