Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amewateua Majaji 10 wa Mahakama Kuu ya Tanzania kuanzia jana Alhamisi, Juni 7, 2012.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi (KMK), Balozi Ombeni Y Sefue jioni ya leo, Ijumaa, Juni 8, 2012, walioteuliwa ni Ndugu Francis Sales Katabazi Mutungi, Ndugu Sam Mpaya Rumanyika, Ndugu Patricia Saleh Fikrini, Dkt. Gerald Alex Mbonimpa Ndika na Ndugu Salvatory Benedict Bongole.

Wengine walioteuliwa kuwa Majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania ni Ndugu Mathew Pauwa Mhina Mwaimu, Ndugu Jacob C.M. Mwambegele, Ndugu Latifa Mansoor, Ndugu John Samwel Mgetta na Ndugu Joaquine Antoinette De- Mello.

Kabla ya uteuzi wake Ndugu Mtungi alikuwa Msajili wa Mahakama ya Rufani Tanzania, Ndugu Rumanyika alikuwa Msajili wa Baraza la Rufani la Kodi, Ndugu Fikirini alikuwa Hakimu Mkazi Mkuu, Ndugu Ndika alikuwa Mkuu wa Chuo cha Sheria Tanzania na Ndugu Bongole alikuwa Naibu Msajili Mwandamizi, Mahakama Kuu.

Ndugu Mwaimu alikuwa Mkurugenzi wa Idara ya Katiba na Haki za Binadamu, Ndugu Mwambegele alikuwa Msaidizi wa Katibu wa Baraza la Mawaziri, Ndugu Mansoor alikuwa Wakili katika Latifa Law Chambers, Ndugu Mgetta alikuwa Hakimu Mkazi Mkuu na Naibu Msajili wa Mahakama ya Rufani na Ndugu De-Mello alikuwa Wakili wa Kujitegemea.

Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
8 Juni, 2012

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...