Mdau Othman Mapara katika matembezi yake  ya hapa na pale mitaani Zenji ili kutafuta matukio kwa ajili ya jamii sehemu za mitaa ya uswahili, alikutana na kijana huyu akiwa katika mchezo na kuku wake aina ya jongoo likiwa na afya njema mashalau... 

Ilibidi asimame na kujuwa kulikoni mambo haya ya Mtu kucheza na kuku... na kuku huyu kufuata amri ya mfugaji wake kijana Khalid Abdalla... na kufahamishwa  kuwa kila jogoo huyu  anapoitwa Chicken huja mbio na kucheza nae. Iibidi Mapara kumuuliza Khalid kulikoni mambo haya tena?

"Haya mafunzo nimemfunza sasa karibu miaka miwili sasa. Wanyama hufanya vile mtu anavyomfunza kuazia mdogo mpaka kukuwa kwake..." alisema Khalid huku akiendelea kucheza na jogoo lake.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 24 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 01, 2012

    huyu ni kijana ???? kweli zanzibar kuna mambo na huo mchezo wa kuku unaitwaje ?? jibu ,muungano udumu. Zebedayo

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 01, 2012

    KWELI ZANZIBAR AMANI IPO MPAKA JOGOO ANACHEZA NA MTU,AAAAAAAAAH KWELI ZANZIBAR MZURI NI HUU MUUNGANO TU NDIO UNAOTUSUMBUWA SISI WAZANZIBAR

    ILA NAO UMEFIKA MWISHO MARA HII LAZIMA WAJE NA VISA

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 01, 2012

    jamani kiswahili tumekisahau siku hizi au?
    Kijana wakati huyu ni jamaa anacheza na jogoo.
    ukisema kijana mimi nadhani yule ambaye si zaidi ya miaka 25-30.

    Ila picha imenichekesha sana. Asante kwa yule aliyetuletea picha

    ni hayo tu.

    Mr Nyamaimewahi Kunikabashingoni

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 02, 2012

    Huyu Jongoo amenona kwa ajili ya MUUNGANO. Mleteni bara muone kama atakatisha Christmas mbili hakiwa hai.

    ReplyDelete
  5. AnonymousJune 02, 2012

    hivi huyu jogoo ikifika idd na krismasi si anajificha? manake ana akili.

    ReplyDelete
  6. AnonymousJune 02, 2012

    Hahahaha

    Niacheni nichekeleeee!!!

    Wazanzibar wananichekesha sana, jamaa amedai Muungano weee Zenji sasa muda wa Mapumziko ya Maandamano anautumia kwa kucheza na Jogooo!

    Au ndio Kampeni zenyewe za Kudai kuvunja Muungano kuwa watu hawana kazi ni kucheza na mifugo tu?

    ReplyDelete
  7. AnonymousJune 02, 2012

    Angalieni sasa!

    Wazanzibar tunakuwa hatuwaelewi madai yenu!!!

    Mkisema Muungano mbaya, sasa huyu Jogoo alivyo nenepa ninyi Zenji hamlimi mahindi, inaonyesha amekula Mahindi ya Mbeya au Iringa ,si ndio neema za Muungano hizo?

    ReplyDelete
  8. AnonymousJune 02, 2012

    Mnaona kwa macho Neena za Muungano hizo?

    Kunenepa kwa Jogoo huyo ndugu zetu Wazanzibar kunaashiria neema adimu za Muungano!

    Mfano tuvunje Muungano puuu, tutawapa mashariti magumu ya kupitisha mchele wetu mpya wa Morogoro, Mbeya na Shinyanga kuingia kwenu Visiwani!

    Je, kwa msingi huo Jogoo anaweza kunenepa kwa mchele wa Indonesia au Iran uliokaa ghalani tokea mwaka 1952?

    FIKIRINI KWANZA KABLA YA KUPANDISHA JAZBA!

    ReplyDelete
  9. AnonymousJune 02, 2012

    Du anagalieni mmeona Wazanzibari mnavyoifaidi Bara?

    Hadi Jogoo ananawiri kwa mchele wa kutoka Bara kiasi hicho?

    ReplyDelete
  10. AnonymousJune 02, 2012

    Ama kweli sisi viumbe wa Mwenyezi Mungu tmepishana sana!

    Jogoo wa Zanzibar anacheza kwa furaha akiwa ameshiba makapi ya nyanya, vitunguu na kabechi kutoka Bara na akiuthamini Muungano ingawa hasemi, huku binaadam (wenye kujitambua) wakiwa wanaupinga Muungano!

    ReplyDelete
  11. AnonymousJune 02, 2012

    Ugumu wa maisha upo wapi Visiwani?

    Angalieni mpaka mtu unapata muda wa ziada wa kucheza na kuku, wakati huku nje Majuu tunafukuzana na muda na tunaumia kwa kubeba Ma box!!!

    ReplyDelete
  12. AnonymousJune 02, 2012

    Binaadam wanatapa tapa kupinga Muungano Zanzibar, Jogoo anhhha anaruka ruka kwa raha zake ndio kanza anaufurahia Muungano!!!!!

    ReplyDelete
  13. AnonymousJune 02, 2012

    YA KWELI HAYA JAMANI?

    ReplyDelete
  14. AnonymousJune 02, 2012

    Uchumi tosha kucheza na kuku,

    haya Zanzibar mjitenge kutoka kwetu Bara pamoja na sekta zingine za mapato yenu ili mkuze mchezo wa kucheza na kuku kama kivutio cha Utalii !!!

    Muungano wa Afrika ya Mashariki na Kenya, Uganda ,Burundi na Rwanda baadae Sudani ya Kusini vinatutosha, bora tuachane na ninyi 'domo wazi'.

    Ya nini malalamiko dhidi yetu?

    ReplyDelete
  15. AnonymousJune 02, 2012

    Uhuru wa nini mnadai kutoka kwetu Bara?

    Zanzibar Uhuru mnao tena wa kumwaga tu!, mpaka mnapata muda wa kuzea kuku!!!!!

    ReplyDelete
  16. AnonymousJune 02, 2012

    Ohhh tunaonewa na sasa hatuna hadi kazi muda mwingi tunacheza na majogoo!!!

    Wakati huo muda anaopoteza hapo angeenda kulima angevuna mazao, angeenda kuvua samaki angepata!

    Kampeni za Kisiasa mchezo?

    Inawezekana Zanzibar wanatuma mapicha kama haya Omani kwa Mkoloni wao Mwarabu ili wapate ushirikiano wa kudai Muungano hauna manufaa kwao!

    ReplyDelete
  17. AnonymousJune 02, 2012

    Hongera Bro. Ulaji huo!!

    ReplyDelete
  18. AnonymousJune 02, 2012

    Zanzibar uhuru ulishaupata tokea umpindue Mwarabu wa Omani mwaka 1964 hadi sasa unafikia kuwa huru hadi unacheza na majogoo na kuku!

    Sisi wa Bara hatutawali Visiwani.

    Huoni wewe na mimi Bara tunashirikiana kimaisha tu?

    ReplyDelete
  19. AnonymousJune 02, 2012

    Mzanzibari unatumia muda mwingi kucheza na kuku badala ya kufanya kazi.

    Baadae unakuwa na njaa malalamiko yote unaelekeza Serikalini, kwenye Chama, Tanzania Bara na kwenye Muungano!

    ReplyDelete
  20. AnonymousJune 02, 2012

    Hadi Majogoo yananona Zanzibar hii yote ni kwa ajili ya neema za Muungano mnao ubeza sasa ngojeni uvunjike muone njaa itakavyowapiga !

    Asalaleeee,

    Mnafikiri mtakuwa na majogoo yanayocheza na yaliyonenepa tena?

    ReplyDelete
  21. AnonymousJune 02, 2012

    Hii yote ni mshikamano na sisi Bara sote tukiwa huru!

    Hali hii ya Uhuru huu wa kucheza na kuku mlikuwa nayo wakati mnatawaliwa na Mwarabu?

    Au mnaweza kuipata kama mtaangukia tena ktk minyororo ya Utumwa na Ukoloni wa Mwarabu?

    ReplyDelete
  22. AnonymousJune 02, 2012

    Kijana si zaidi ya miaka 25-30

    Inawezekana jamaa ni kijana lakini 'amezeeka' kutokana na hizo shida wanazodai kuletewa na Tanzania Bara na Muungano!

    ReplyDelete
  23. AnonymousJune 04, 2012

    neema gani ya muungano hii ni kheri yetu na baraka zetu za nchi yetu zanzibar ndo maana kanenepa jogoo, na bora kucheza na jogoo kuliko kucheza na akili za watu kuwafanya mazuta(zumbu kuku) kwa kujificha katika kichaka cha muungano

    hatuutaki muungano wazanzibari tunataka amani yetu ndo maana tunacheka na jogoo hatuna shari na mtu lakini mnatuleta balaa zenu hatuzitaki

    nendi mkaungani na kongo, uganda,malawai etc not us any more

    ReplyDelete
  24. AnonymousJune 05, 2012

    Mdau wa 23 hapo juu Anony Mon Jun 04, 01:51:00 PM 2012

    MUUNGANO HAUVUNJIKI WALA HAUFI...UTAKUFA WEWE NA NJAA ZAKO!

    FANYA MPANGO UOMBE PASIPOTI YA OMANI MAPEMA KWA KUWA MATARAJIO YAKO KAMWE HAYATOTIMIA!!!

    ZANZIBAR IKIFANIKIWA KUJITENGA ''NITAKUNYA'' SAA 7 MCHANA MJINI POSTA BARABARANI, KITUO CHA BASI AU KWENYE STENDI YENU YA MABOTI YA ZANZIBAR HUKU DAR PALE POSTA BAHARINI !!!!

    MAJOGOO YENU YANASHIBA KWA NEEMA ZA BARA ZA MUUNGANO NINYI MNA NJAA KALI SANA , TENA HAMLIMI WACHA MAHINDI NA VYAKULA ,MNA NJAA HATA ZA MBOGA MBOGA VITUNGUU ,NYANYA, HADI KABECHI NA PILI PILI MNAAGIZA BARA!

    THUBUTU!!!

    KUJITEGEMEA MTAWEZA NINYI?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...