Spika wa Bunge akisaini kitabu cha maombolezo alipofika nyumbani kwa mtoto wa marehemu Ilala , Dar es salaam kuhani msiba wa aliyekuwa Mbunge wa Ludewa na Naibu Spika wa Bunge katika Bunge la Tanzania kuanzia mwaka 1990 hadi 1995. Marehemu Mathias Kihaule alifariki Jumapili katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili alipokuwa amelazwa akisumbuliwa na maradhi ya Kichwa na anatarajiwa kuzikwa kijijini kwakwe Ludewa leo.
Mhe. Spika akiwa na mjane wa Marehemu Mathias Kihaule Bi. Leonia Kihaule alipofika kuwafariji Nyumbani kwao Ilala jana jioni. aliyepembeni ni Ndugu wa Marehemu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 07, 2012

    Mila zetu ukienda msibani lazima ufunike kichwa na uvae kanga mbona mama yetu hana? kwani hiyo kanga ukiiweka kwenye pochi ni tabu? Tudumishe mila zetu haswa hii hapa

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...