Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mh.Lazaro Nyalandu alitembelea Msitu wa Hifadhi ya Kazimzumbwi ulioko wilaya ya Kisarawe mkoani Pwani kujionea uharibifu wa mazingira unaofanywa na kikundi cha watu wanaotaka kujitwalia maeneo ndani ya msitu kuanzisha makazi yao.
akizungumza baada ya kujionea uharibifu huo na kukagua mipaka kama inavyoelekezwa na Tamko la Serikali no 306 la Septemba 1954 ambalo lilianzisha rasmi msitu huo wa hifadhi kwa ajili ya kulinda na kuhifadhi vyanzo vya maji kwa wakazi wa mikoa ya Dar es salaam na Pwani na vizazi vijavyo.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mh.Lazaro Nyalandu akipitia ramani ya eneo hilo la Msitu wa Kazimzumbwi.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mh.Lazaro Nyalandu akipatiwa maelezo na Mmoja wa viongozi wa Wilaya ya Kisarawe juu ya Msitu wa Kazimzumbwi.
mbona hakuna msitu?
ReplyDeleteMhe Nyalandu, angalieni pia wajibu wa serikali za vijiji na halmashauri yake (kijiji). Mkitaka ninyi ndiyo mje kutokea taifani kulinda maeneo ambayo yako chini ya Halmashauri za Wilaya, ambako yupo hata DNRO, basi mtakuwa mnakuta hali kama hiyo. Wapeni serikali za vijiji, na halmashauri za Wilaya husika, nafasi ya kuwajibika. Ndiyo maana tulizichagua serikali hizo ati!
ReplyDeleteMzoefu wa uongozi.