Mahakama ya Kisutu jijini Dar es Salaam leo ilifurika umati wa watu waliofika kufuatilia kesi inayomkabili Rais wa Chama cha Madaktari Tanzania (MAT), Dk. Namala Mkopi (pichani).

Dk. Mkopi amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam ambapo alisomewa mashitaka mawili.

Mashitaka hayo ni kukiuka amri halali iliyotolewa na Mahakama Kuu ya Tanzania, Divisheni ya Kazi iliyomtaka yeye na wanachama wake kutoshiriki au kujihusisha na mgomo wa madaktari na kuhamasisha mgomo kinyume na amri hiyo.

Dk. Mkopi alisomewa mashitaka hayo leo na Wakili wa Serikali Mwandamizi Tumaini Kweka akisaidiana na Wakili wa Serikali Ladislaus Komanya,mbele ya Hakimu Mkazi Faisal Kahamba.

Wakili Kweka akisoma mashitaka alidai kati ya Juni 26 na 28, mwaka huu, Dar es Salaam, mshitakiwa akiwa Rais wa MAT hakutii amri halali ilitolewa na Mahakama Kuu ya Tanzania, Divisheni ya Kazi ambayo ilimtaka atoe tangazo kwa kupitia vyombo vya habari kwa wanachama wake kutoshiriki au kujihusisha na mgomo.

Amri ambayo ilitolewa na mahakama Juni 22, mwaka huu.

Shitaka la pili, Dk. Mkopi anadaiwa Juni 27, mwaka huu, Dar es Salaam, waliwashawishi wanachama wa chama cha MAT Tanzania Bara kushiriki mgomo ikiwa ni kinyume na amri iliyotolewa na Mahakama ya Kazi, Juni 22, mwaka huu.

Dk. Mkopi alikana mashitaka hayo, ambapo upande wa mashitaka ulidai upelelezi haujakamilika.

Mawakili wa Dk. Mkopi Isaya Matambo, Dk. Maurid Kikondo, Dk. Gaston Kenedy na Dk. Rugemeleza Nshala waliomba mteja wao apatiwe dhamana kwa kuwa mashitaka yanayomkabili yanadhaminika.

Hakimu Kahamba alitoa masharti ya dhamana ambayo mshitakiwa awe na wadhamini wawili waajiriwa wa serikali au kutoka taasisi inayotambulika kila mmoja atatia saini dhamana ya sh. 500,000.

Wakili wa Serikali aliiomba mahakama izingatie kifungu cha 148(6) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai (CPA), kinachoelekeza masharti ya nyongeza wakati wa kutoa dhamana ambayo ni mshitakiwa kuwasilisha polisi hati za kusafiria na kutotoka nje ya mkoa husika bila ya kibali cha mahakama.

kesi hiyo imeahirishwa hadi Agosti 6, mwaka huu, kesi itakapotajwa kutokana na kutimiza masharti hayo Dk huyo yuko nje kwa dhamana.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 31 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 10, 2012

    God bless you Dr. Mkopi and your fellow doctors!!
    Etienne

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 10, 2012

    Poleni Watz, hivyo watu wakidai haki zao wanashitakiwa, myself i think mtawasababisha wagome tena na ndugu zetu wanapokufa serikali haitakuwepo kutusaidia kulia, maana wagonjwa wa vigogo wote wanapelekwa nje ya nchi kutibiwa. Government u should give them what they want!!!!, angalieni wafanyakazi wa benki kuu, na wengine wanavyopewa hadi maziwa ya kuwapelekea watoto wao wakati hawanusi mavi,mkojo,damu,usahau or hawana risk kubwa kama wafanyakazi wa afya!!!!

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 10, 2012

    That is not the only solution to tackle their concerns. Something should be done by the government by having a dialogue on how to solve all their concerns. This action on suing their president will act like a catalyst of making them more and more demoralized.

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 10, 2012

    Is this the start of the Tanzanian Revolution?

    ReplyDelete
  5. AnonymousJuly 10, 2012

    JAMANI MGOMO SI TUMEAMBIWA UMEISHA! SASA HII KESI YA NINI TENA?

    ReplyDelete
  6. AnonymousJuly 10, 2012

    kuto poteza hela za walipa kodi mnaweza kumuua na huyo ili shuguli za kujenga uchumi ziendelee, tumechoshwa na hawa wapuuzi njaa zao wanataka kutuletea tz nzima bana

    ReplyDelete
  7. AnonymousJuly 10, 2012

    acha upumbavu angekua ni mama yako ungesema hivyo

    ReplyDelete
  8. AnonymousJuly 11, 2012

    Ningefurahi kusikia kutoka kwa wataalam wa sheria kama mahakama ilitenda haki kwa kutoa amri ile, na kama ilizingatia sheria pia ama ilitumia ubabe. Baada ya kuelimishwa hilo nitatoa comment yangu.

    ReplyDelete
  9. AnonymousJuly 11, 2012

    Hii ndo safi sana, siyo ile ya kuwapiga au kuwaua hapana, ukisha kataza kitu sasa subiri anayekuwa m'bishi ndo huyo unampandisha kizimbani na wala siyo kumpiga au kumuua hapana.
    Na huu ndo ukomavu wa akili.

    ReplyDelete
  10. AnonymousJuly 11, 2012

    Mgomo umeisha..kesi za nini?

    David V

    ReplyDelete
  11. AnonymousJuly 11, 2012

    Sijui kama Dr. Mkopi ana uwezo wa kuwazuia madaktari kugoma pia baada ya amri ya mahakama kutolewa, alisikika Dr mmoja mwanamke kiongozi wa madaktari bingwa akisema kwamba madaktari bingwa nao wanagoma sasa huyo ambaye ametoa tamko baada ya amri ya mahakama itakuwaje? mimi nadhani njia pekee ni kukaa na madaktari na kukubaliana yanayowezekana njia hizi nyingine zote ni kukosa busara na kuongeza matatizo.

    ReplyDelete
  12. AnonymousJuly 11, 2012

    Mahakama ni mahakama bwana ndio utawala wa kisheria. Watanzania hata mkikamatwa mmemgonga mtu mnataka kutoa fedha yaishe. Kudharau kauli ya mahakama ni kosa la jinai. Someni humu mtandaoni. Watanzania ni wajinga. Bora umpige kiatu raisi utasamehewa kuliko kupinga hukumu ya mahakama kuu. Katiba isomeshwe tokea darasa la kwanza watu wajue mipaka ya vitendo vyao. Ushenzi sio kabila ila matendo ya watu. Watanzania wengi wamesoma lakini hawajaelimika, hasa madaktari.

    Nyinyi mnaowapendelea hamjaugua mkalazwa Muhimbili halafu daktari akakuacha bila kukutibu bila ya kumlipa chochote. Mimi yamenikuta, sina hamu nao kabisa, ni wauwaji.

    ReplyDelete
  13. AnonymousJuly 11, 2012

    Hata wakipewa vifaa, mamilioni ya fedha za mshahara ndio watadai zaidi kwa wagonjwa wakiambiwa kwamba vifaa vinavyotumika ni vya kitaalamu sana. Pesa ilimtosheleza nani, tajiri kila siku anataka zaidi. Pale Moi unalipa fedha nyingi, Daktari anakaa siku mbili hakupita, yuko kwenye hospitali yake binafsi.

    ReplyDelete
  14. AnonymousJuly 11, 2012

    Wewe Etienne wacha unafiki. Wewe unadhani kule kwenu Rwanda hawa madaktari wangelithubutu kugoma? God will never bless killers! God will punish severely all murderers!

    ReplyDelete
  15. AnonymousJuly 11, 2012

    Hivi kwa wale maenda hospitali huyo ni daktari wa hospitali gani? mbona wale madaktari ninaowajua wa Ilala, Temeke , Amana na Muhimbili ninaopishana nao wakichacharika na kazi huyu siwahi kumwona. Watu kama hawa wala siwafanyakazi wazuri kutwa wanatafuta maslahi yao zaidi kuliko umoja wa kitaifa na kudai haki kwa amani. Wanavyokufa watu kwa mgomo anafurahia sijui hana ndugu hapa tz? NIDA harakisha vitambulisho vya uraia ili tujuane.

    ReplyDelete
  16. AnonymousJuly 11, 2012

    duniani kitu wema, wema haujaonekana,
    yamebakia mateso, waafrika (wanyonge) ndio wauwawa,
    ni mashaka yaanza hivyo, wema hawana maisha.
    By the late Patrick Balisidya

    ReplyDelete
  17. AnonymousJuly 11, 2012

    HIVI HUYU NI DAKTARI KWELI, AU NI WALE WANAOTAFUTA MASLAHI BINAFSI UKITAZAMA HATA SURA YAKE KAMA KIBAKA TU, HANA WITO WOWOTE HUYU NI KATI YA WALE WALIOKUWA VINARA WA MIGOMO UDSM, SASA BADO WANAWAVURUGA WALE WENYE WITO WAO. SIJAWAHI KUMUONA SIJUI ANAFANYIA HOSPITALI GANI AU NI AKINA NANIHII KIONGONZI WA MGOMO

    ReplyDelete
  18. AnonymousJuly 11, 2012

    ukiona dakitari hafanyi haki kasomee udakitari au shawishi watoto wako wachukue fani hii sio kukwepa masomo ya sayansi jamani.

    ReplyDelete
  19. AnonymousJuly 11, 2012

    We unayejiita ETIENNE sidhani kama ni M-TZ halisi! Nadhani uko nje ya nchi na kama ni M-TZ. Ungekuwa hapa ungepita katika hospitali na ukaona huo mgomo ulivyoua watu! Mie mke wangu na mwanangu walifariki kwa kukosa kufanyiwa operation ya uzazi leo unaandika hivyo kweli!? Ningekuona kwa macho nadhani hata nami ningenyongwa kwa sababu ningekuua kabisa!! tena wale wote wanaounga mkono wasithubutu kwani hawakufiwa na watu wao wa karibu!

    ReplyDelete
  20. AnonymousJuly 11, 2012

    OMG we Anony wa (Wed Jul 11, 10:29:00 AM 2012) hapo juu. USHINDWE NA ULEGEE KABISA. You cant judge a book by its cover. How would you say he is Kibaka jamani? This is sad, sad, sad. Ndio nyie wa kukatisha watu tamaa katika maisha yao. Go..Go..Dr. Mkopi. Good luck in what you are facing bro. Achana na hawa wanaokuona wewe Kibaka. Hivi angekuwa kaka yako ungemuita Kibaka. NonSense kabisa!

    ReplyDelete
  21. AnonymousJuly 11, 2012

    Nadhani sarikali sasa ifanye kile ambacho Watza wengi tunakitarajia.

    Waoneshe kwamba tumewaamini na kuwapa mamlaka sio kuchezewa chezewa na CDM na associates wao!

    ReplyDelete
  22. AnonymousJuly 11, 2012

    Acheni unafiki, nyie mnaomsema Huyo Dr. Wanahaki ya kudai maslahi yao. Ni kweli kuna Taasisi nyingi za Serikali pia TRA wanapewa pakiti za maziwa, wakati kazi wafanyazo si za RISK kiasi hicho, WHY NOT DOCTOR!!!? ambao wakati wote na mahali popote mikono yake inaogelea kwenye MADIMBWI YA DAMU.

    Nchi hii hata kama inaongozwa na utawala wa Sheria, haimaanishi ndio kutisha wananchi. Hebu tumuogope Mwenyezi Mungu na tuambiane ukweli kama huu;

    (1) Wabunge wetu mpaka sasa wana lipi jipya? Wanalipwa mishahara minono na allowance kibao, pia wakiumwa wanapelekwa nje, kwa nini tusipiganie haki ya kuwa na wao pia watibiwe hapa?

    (2) Naamini Dr huyu alichaguliwa na wenzie, kuwaongoza, ameaminika kwa hiyo asimamapo ni kwa niaba ya wenzie. Mbona tunapiga kelele hali ngumu hali ngumu, hali Landcruiser kibao za Serikali ziko mitaani zimezagaa kwenye mambo yasiyo ya msingi kwa mfano sasa hivi zinapeleka watoto shule, mama sokoni, kwenye mashamba, kwa vimada. Kwani tusiyauze kwa asilimia 90 na kuwakopesha magari ili tubane matumizi na kupata mishahara ya madaktari na waalimu.

    MNYONGE MNYONGENI, HAKI YAKE MPENI.

    HAKUNA KAZI YA WITO HAPA, MBONA NYIE MMEKWENDA DODOMA NA ALLOWANCE KIBAO?

    ReplyDelete
  23. AnonymousJuly 11, 2012

    WATANZANIA AMKENI. HAWA MADKTARI SIO WANATAFUTA MASLAHI YAO TU, WANACHOPIGANIA NI SERIKALI KUJALI SEKTA NZIMA YA AFYA. KUANZIA WAO WENYEWE KUJALIWA NA KUTHAMINIWA, PIA WANATAKA VIFAA BORA VYA KUKUTIBU WW NA FAMILIA YAKO KWA UFANISI ZAIDI.
    WATANZANIA BADO HATUJUI MAANA YA SACRIFICE. LEO HAWA MADAKTARI WAKISACRIFICE , PAMOJA NA WW KUATHIKA KWA HILO, KESHO, WW AU MWANAO NDIO WATAKAO NUFAIKA KAMA SERIKALI ITATIMIZA MATAKWA YAO.

    ReplyDelete
  24. AnonymousJuly 11, 2012

    mimi nashangaa watu wanaowatetea hawa madaktari,hatukatai madai yao ila mfumo wanaoutumia ni wauwaji wakubwa na wanakiwa kulipia haya matokeo ya vurugu zao,hawa watu wanasomeshwa bure hawana nusu ya mkopo mpaka wanamaliza na bado wakiagiza magari nje ya nchi wanapewa exemption hawalipi ushuru bado hawaridhiki wanatutesa tu watanzania
    Kuna hawa wanaojifanya watetezi wa haki za binadamu ndio wanaowaunga mkono kitu cha ajabu wanaona watu wanakufa sasa hao wanaokufa hawako kwenye hizo haki za binadamu?au wako kwenye haki za kunguni??Nyie watu wa haki za binadamu ningekuwa na mamlaka ningewafungia hivyo vi ofisi vyenu wapuuzi kabisa nyie

    ReplyDelete
  25. AnonymousJuly 11, 2012

    Mi kwa mtazamo naona madaktari sheria haiwaruhusu kugoma, sekta zote kwenye nchi zinaumuhimu wake. wadai haki zao bila kusabisha maafa tena ilibidi wt waliogoma wakamatwe na warudishe hela zt za walizosomeshewa

    ReplyDelete
  26. AnonymousJuly 11, 2012

    Madaktari wana haki ya kudai maslahi bora ... lakini kitendo cha kuacha watu wafe ... ili serikali iwape haki zao ... mie kwa kweli kimeniuma saaaana ... nakuambia hakuna kitu kizuri kama kumjali mtu .... PESA INAPITA ... IKO SIKU ... UNA PESA .. LAKINI UKAKOSA HUDUMA MUHIMU .... PESA SIO KILA KITU ... UTU KWANZA ...

    TUWE NA UTU NDUGU ZANGU ... UHAI WA MTU HAUNUNULIWI NA KITU ...

    KWANI UTAKUFA NA UTAACHA PESA ZOOTE NA NDUGU WATAZIPIGANIA ..... LAKINI SIFA/ MATENDO YAKO HAYATASAULIKA .... UTU KWANZA MENGINE YANAFUATA.....

    ReplyDelete
  27. AnonymousJuly 12, 2012

    ...WAPO WALIOKUWA TAYARI KUONA WAGONJWA WAKITESEKA ILI MRADI TU MASLAHI YAO KWANZA...HUYU KAMWE HAWEZI KUITWA DAKTARI NI MUUAJI TU.

    PILI, PAMOJA NA KUJUA FANI YAO LAKINI IMEONESHA MADAKTARI WETU BADO WANAUPEO MDOGO WA KUFAHAMU WAJIBU WAO KWA MUJIBU WA FANI UTABIBU. KWA VILE NAAMINI KUWA HII FANI INA PROFESSIONAL COUNCIL BASI MZIZI WA FITNA UTAKATWA HUKO...N AIKIBIDI WATAKAOBAINIKA WALIKWENDA KINYUME NA MAADAILI YA FANI HIYO BASI WAFUTIWE LESENI ZAO KABISA...NI HERI KUWA NA MADAKTARI WACHACHE WANAOJALI KAZI YAO KULIKONI KUWA NA MAMIA WASIOTAKA KUFUATA TARATIBU ZA FANI HIYO

    NDUGU YANGU MKOPI ALISHINDWA KUTOFAUTISHA BAINA YA MTAALAM NA MWANASIASA...ALIPOTAKIWA KUTII AMRI YA MAHAKAMA, HAKUTAKIWA KUFANYA UBABE KAMA WALIVYOWAFANYIA WAGONJWA...BALI NI KUFUATA MKONDO ULEULE WA MAHAKAMA AIDHA KWA KUTII AMRI AU KUKATA RUFAAA...KUSHINDWA KUTAMBUA HILI KUMEONESHA UDHAIFU MKUBWA SANA

    ReplyDelete
  28. AnonymousJuly 12, 2012

    Jamani wale wote wenye akili na'exposure' ya mambo ya kidunia nauliza: Ni kwa nini ktk nchi zilizoendelea madaktari na manesi wanapata mishahara mikubwa SANA ukilinganisha na wafanyakazi wa sekta nyingine ? Utaratibu huu pia unaonekana ktk baadhi ya nchi za kiafrika. Na kwa nini utaratibu huu umekubalika kwa wananchi wao?
    Tanzania kwa nini karani wa benki kuu au TRA analipwa kuliko daktari, tena wengine wanadiploma tu?
    Uganga huu wa kisasa tumeletewa toka ughaibuni lakin wao hawang'ang'anii kuwA kazi ya afya ni wito hivyo posho stahili iwe ndogo. Kwa nini?
    Watanzania kwa nini hatupendi afya zetu ziwe mikononi mwa watu walioridhika kimapato na kimazingira ya kazi?
    Kwa nini udaktari unasomea muda mrefu, miaka mitano hadi sita?
    Fani hii kwa nini ni ngumu kimasomo?
    Jamani kwanini fani hii ni ya ajabu na heshma kote ulimwenguni kasoro Tanzania ?
    Kwanini...
    Mchunguzi.

    ReplyDelete
  29. AnonymousJuly 12, 2012

    hana sura ya udaktari

    ReplyDelete
  30. AnonymousJuly 12, 2012

    Jamani wale wote wenye akili na'exposure' ya mambo ya kidunia nauliza: Ni kwa nini ktk nchi zilizoendelea madaktari na manesi wanapata mishahara mikubwa SANA ukilinganisha na wafanyakazi wa sekta nyingine ? Utaratibu huu pia unaonekana ktk baadhi ya nchi za kiafrika. Na kwa nini utaratibu huu umekubalika kwa wananchi wao?
    Tanzania kwa nini karani wa benki kuu au TRA analipwa kuliko daktari, tena wengine wanadiploma tu?
    Uganga huu wa kisasa tumeletewa toka ughaibuni lakin wao hawang'ang'anii kuwA kazi ya afya ni wito hivyo posho stahili iwe ndogo. Kwa nini?
    Watanzania kwa nini hatupendi afya zetu ziwe mikononi mwa watu walioridhika kimapato na kimazingira ya kazi?
    Kwa nini udaktari unasomea muda mrefu, miaka mitano hadi sita?
    Fani hii kwa nini ni ngumu kimasomo?
    Jamani kwanini fani hii ni ya ajabu na heshma kote ulimwenguni kasoro Tanzania ?
    Kwanini...
    Mchunguzi.

    ReplyDelete
  31. AnonymousJuly 12, 2012

    Hawa madaktari kwanza mishahara yao wawelipwe nusu mshahara wanaogoma au wafukuzwe kazi kabisa,masikini wakubwa nyie.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...