Kwa sababu ya Poor copyrights and Income Managment , naamini Serikali Huenda ikawa inapoteza Fedha Zisizopungua Shillingi za Kitanzania Million Hamsini (50,000,000.00) kwa kila watanzania Millioni Moja (1,000,000) wanatumia Simu au Kuingiza nyimbo kwenye simu au kurekodiwa kwenye CD.
Hii ni kwa hesabu zangu za darasa la nne :-
Nyimbo sasa hivi zinaingizwa kwa 200/= hadi 500/= kwenye CD au SIMU / Per Song.
Hivi kama kungekuwa na utaratibu wa kusimamia hizi kazi za wasanii kwa asilimia ndogo tu, unafikiri vijana wangekimbia mashamba?
Banana, Dully, Diamond, Ally Kiba na wengineo wengi wangekuwa na mashamba makubwa na wala kusingekuwa na shida ya chakula.
Anyway, back to my subject.
Kama Kukiwa na usimamizi mzuri naamini kila msanii anaetoa nyimbo na ikasimamiwa vizuri na Serikali au wasimamizi wengine watakaolindwa na serikali basi kila nyimbo inaweza (Rate Ya Watu 1,000,000 tu) :-
Kumpatia Muuzaji / Anayeweka nyimbo kwenye simu : Tsh 150 - 300 kwa nyimbo.
Kumingizia Kipato Msanii : Tsh 50,000,000 kwa nyimbo x (1,000,000 x Tsh 50).
Kuiingizia Kodi Serikali : Tsh 50,000,000 kwa nyimbo = (1,000,000 x Tsh 50).
Ni Hayo Tu.
TAFAKARI - CHUKUA HATUA.
Dream on ndugu. Serikali cant even regulate its major source of income, taxes, and you are thinking about songs and copy rights? Nyimbo zenyewe unaongelea bongo fleva which rarely portray "Tanzanianism". I praise you for the simple math to show when magnified can made much difference but music industry (and economics behind it) is tougher than you can simply think.
ReplyDeleteSiyo "kila nyimbo" bali ni "kila wimbo."
ReplyDeleteSasa zikiwa nyingi utaziitaje? Utaziitta "zimbo"?
Kuwaiga Wakenya na Kiswahili chao kibovu ni ujuha. Hii ni lugha yetu tuacheni uzungukuku.
Matinyi.
AHSANTENI, HAYA NDIO MAMBO YA KUYAFUATILIA KWA KUTUMIA SHERIA, WENZENU WANAPATA FEDHA KIULAINI KWA KUTUMIA NYIMBO ZENU MLIOUMIA KUZITUNGA NA KUZIIMBA ZIKAPENDWA, NAWAKUMBUSHA NYIMBO NI NYINGI N MMOJA NI WIMBO, KICHWA CHA HABARI HAKIKO SAWA.
ReplyDeleteNashukuru Matinyi kwa somo,
ReplyDeleteHuwa nakereka sana utamsikia unasema hii nyimbo naipenda sana! badala ya wimbo.
Tafadhali!
Ukiwa mmoja ni WIMBO na zikiwa nyingi ni NYIMBO
Tuko vizuri katika kuendeleza mijadala sio kuanzisha!
ReplyDeletesesophy
ndo maana wabongo atuendelei mtu katoa hoja yakunufaisha watanzania wote, badala yakufikiria jinsi ganiyakufanya ili iweze kufanikiwa mnaanza kupinga nakumsaisha kiswahili chake, kweli tutasonga kweli? jamani naomba tuwe watu wakufikiri na kuwapositive, negativity doesn't take us anywhere...
ReplyDeleteWewe Matinyi hacha hizo. Kwa hiyo Wakenya Kiswahili siyo lugha yao? Haluu... Wakenya na Watanzania wote wanakosea kwenye kuzungumza lugha fasaha. Si ajabu kuna Watanzania wengi tu walianguka mtihani wa Kiswahili wakati ndio "lugha mama"
ReplyDeleteHivyo usiwajumlishe watu. Sema fulani... kwa maana "Wakenya" hawazungumzi lugha kwa pamoja. Vivyo hivyo "Watanzania" hawazungumzi lugha kwa pamoja.
Kuna wanaozungumza lugha fasaha na kuna ambao wanakosea.
Na wewe Matinyi hakuna neno 'zungukuku'... ni zumbukuku.
ReplyDeletePia namkumbusha mdau hapo juu kwamba hakuna neno "hacha" bora ungesema "acha" au "wacha".
ReplyDeleteHata hivyo mbona wabongo kuibiwa mlishaona ni sehemu ya utamaduni wenu? Mnawachoma vibaka wanaowaiwaibia simu za sh 50,000/= mnawaacha wanaowaibia mabilioni! Shame on you!