Waziri wa Mamboya ndani wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Emanuel Nchimbi alifikakatika Eneo lililohifadhiwa Maiti wa Ajali ya Meli ya Skagit ili kutambuliwa na Ndugu zao na Kupata maelezo kwa Daktari Kiongozi hayupo pichani Hapo katika Viwanja Vya Maisara Zanzibar.
Baadhi ya Maiti zilizookolewa kutoka katika Meli iliozama na kukosa watu wake zikipelekwa kuzikwa na Serikali katika Eneo la Kama lililotayarishwa makusudi kwa ajili hio.
Balozi wa Marekani Nchini Tanzania Learnhat Alfonso wakatikati akionekana na huzuni Baada ya kuziona Maiti zilizookolewa katika Meli iliozama hapo jana katika Bahari ya Chumbe Zanzibar.Balozi alifika katika Viwanja vya Maisara ili kuona namna shughuli za kushughulikia maiti zinavyoendelea.

BOFYA HAPA KUONA PICHA ZINGINE

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 6 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 20, 2012

    Jamani Tanzania viongozi milopewa dhamana mtatumaliza kwa sababu ya rushwa. Iweje meli iruhusiwe kubeba abiria bila hata maboya ya kujiokolea? Halafu meli haizami kama jiwe ilikuwaje hii ikazama haraka namna hiyo? Hata kutuma ujumbe wa dharura kuomba msaada ilishindikana? Watu wenye pesa wanatumia pesa zao kwa kutoa rushwa na kupewa leseni za kusafirisha abiria bila kujali usalama na maisha ya abiria hao. Hayati Baba wa Taifa alisema "Ubepari ni Unyama" na huu nao ni unyama. Rushwa itaendelea kuleta maafa kwa wanyonge Tanzania. Kuzama kwa meli sasa inaelekea kuwa kitu cha kawaida tu.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 20, 2012

    Siku moja tu haitoshi kusema kwamba maiti za wahanga wamekosa ndugu!

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 20, 2012

    eeeh mungu wetu .... this is crazy!

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 20, 2012

    R.I.P. kwa wale wote waliohusika. Swali humu ndani, hivi maiti INAOKOLEWA au KUOPOLEWA toka kwenye maji? Msinielewe vibaya mie elimu yangu ya 1979 labda sijaelewa vizuri tu.

    ReplyDelete
  5. AnonymousJuly 20, 2012

    Inahuzunisha sana jamani. lakini mbona hawa watu wanazikwa kwa imani moja tu? kila anayekwenda Zanzibar ni wa imani hiyo? just curiosity to know

    ReplyDelete
  6. AnonymousJuly 20, 2012

    Maiti inaopolewa toka kwenye maji, majeruhi wanaokolewa toka kwenye maji.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...