Uongozi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili unawatangazia Madaktari wote ambao hawafiki kazini kuwa wanatakiwa kurudi kazini mara moja kwa kujiorodhesha majina yao kwa wakuu wao wa Idara.

Aidha, tangazo hili pia linawahusu Madaktari wote wanaokuja kazini lakini hawafanyi kazi, nao wajiorodheshe kwa wakuu wao wa Idara.

Wakuu wote wa Idara wanatakiwa kuwaorodhesha Madaktari wote watakaofika kazini kuanzia leo (2/Julai/2012) na kuhakikisha wanafanya kazi kwa mujibu wa sheria, kanuni, na taratibu zilizopo.

Zoezi hili litafungwa kesho tarehe 3 Julai 2012 saa tatu asubuhi.

Tangazo hili haliwahusu Madaktari walio katika Mafunzo kwa Vitendo (Interns).

Dr. Marina Njelekela,
Mkurugenzi Mtendaji
Saa 06:00 Mchana

Nakala: Wakurugenzi - Kwa usimamizi

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 5 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 02, 2012

    kwa nini msiwafukuze tu maana hawataki kazi mkiwalaimisha watatuua jamani,mfano mtu anaumwa malalia anapasuliwa kichwa nk,hebu waacheni wapumzike kwanza watulize hasira zao,pia muwape hela awanazotaka kama mnazo kama hakuna tafuteni kwanza ndipo muwaite

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 02, 2012

    ....na mkuu wangu wa idara amegoma....

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 02, 2012

    Safi sana Madaktari mnatakiwa mrudi kazini na kufanya kazi, tunaiomba serikali iwafukuze kazi wale wote watakaokaidi amri hii.

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 02, 2012

    Safi sana boss, wasipotii fukuza, kudadadeki...

    ReplyDelete
  5. AnonymousJuly 02, 2012

    Binafsi sioni sababu ya watumishi hawa wa umma kubembelezwa kupita kiasi, ni bora serikali iwape talaka ili wakatafute mume mwingine atakaeweza kuwatimizia haja zao zote.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...