UTANGULIZI

1.            Mheshimiwa Spika, tarehe 12 Juni, 2012 tulianza Kikao cha Kwanza cha Mkutano wa Nane wa Bunge lako Tukufu na leo tunafikia tamati. Ni jambo la kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutuwezesha kuhitimisha shughuli zote zilizopangwa kwa amani na salama. Mkutano huu ulikuwa mahsusi kwa ajili ya kuwasilisha, kujadili na hatimaye kupitisha Bajeti ya Serikali ikiwa ni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Wizara, Mikoa na Taasisi mbalimbali.

2.            Mheshimiwa Spika, napenda niwashukuru Waheshimiwa Wabunge kwa kutumia muda wote wa Mkutano huu kwa ufanisi mkubwa kuchangia hoja zinazolenga katika kujenga na kusaidia Taifa letu. Napenda kuchukua nafasi hii kuwapongeza Waheshimiwa Wabunge wote kwa mwamko huo mzuri ambao bila kujali itikadi za Vyama umetoa changamoto kwa Serikali katika kutekeleza malengo tuliyojiwekea ili kuleta maendeleo ya Nchi yetu. Ninawashukuru sana kwa michango yenu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...