Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akijumuika na waumini wa dini ya Kiislam, katika swala ya Magharibi wakati alipojumuika na waumini hao katika Futari ya pamoja aliyowaandalia na kufuturu nao Migombani Unguja mjini Zanzibar jana Agosti 01, 2012
Wake wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Zakhia Bilal (wa pili kulia) na Mama Asha Bilal (katikati) wakijumuika na waumini wa dini ya Kiislam, wakati wa futari ya pamoja iliyoandaliwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, kwa waumini hao iliyofanyika Migombani Unguja, mjini Zanzibar jana Agosti 01, 2012.
  
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na baadhi ya Waumini wA dini ya Kiislam, baada ya kufuturu nao futari ya pamoja aliyowaandalia Migombani Unguja mjini Zanzibar jana, Agosti 01, 2012. 
Mke wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Asha Bilal, akipiga picha ya pamoja na baadhi ya kinamama, baada ya kushiriki nao katika futari ya pamoja iliyoandaliwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, iliyofanyika jana Migombani Unguja mjini Zanzibar.
Mke wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Zakhia Bilal, akipiga picha ya pamoja na baadhi ya kinamama, baada ya kushiriki nao katika futari ya pamoja iliyoandaliwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, iliyofanyika jana Migombani Unguja mjini Zanzibar. Picha na Muhidin Sufiani-OMR

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. pesa za kufuturisha anazitoa wapi. Nadhani hizo si pesa za walipa kodi

    ReplyDelete
  2. Kwani ni asiwe na pesa za kufuturisha? Hakuna wana siasa maskini Tanzania.

    ReplyDelete
  3. umecheki jumba hili halafu unauliza pesa anazipata wapi, huyu jamaa msomi na alikuwa hataki mambo ya siasa alikuwa anataka kuondoka ndani ya nchi wakamzulia pasipoti yake sasa unauliza nini utumbu utumbo tu eti pesa kapata wapi kisomi chake tosha kuwa pesa akindondoka majuu noti noti anachezea kiyama ndo maana ana totoz mbili mmoja nyeusi mmoja nyeupe nyeupe hapendi taabu

    ReplyDelete
  4. Inshllah Sheikh Bilal futari aliiandaa vyema sana Mwenyezi Mungu atamlipa!

    Ameeeen!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...