Mstahiki Meya wa manispaa ya Ilala, Jerry Silaa akikabithi fomu za kugombea nafasi ya ujumbe wa UVCCM-NEC kwa Katibu wa UVCCM mkoani Mwanza,Bw Elias Mpanda katika ofisi za CCM mkoa. Jijini Mwanza. Mstahiki meya Manispaa ya Ilala Bw Jerry Silaa anagombea nafasi ya ujumbe wa UVCCM-NEC ngazi ya taifa.Mstahiki meya aliweka wazi nia yake ya kutaka kuwawakilisha vema vijana wa kitanzania kwenye UVCCM-NEC na aliwaasa vijana wengine kushiriki kwenye mchakato huo na huku akisisitiza kwamba yuko tayari kufanya kazi kokote nchini kwa maslahi ya wananchi, vilevile meya aliwaasa viongozi wote kuwajibika na kutimiza ahadi zao walizozitoa kwa wananchi na kwa kuweka mbele maslahi ya taifa na sio yao binafsi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Huyu mtoto wa Dr. Slaa au ndugu yake???

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...