Si ingine bali ni Ngoma Africa band aka FFU,bendi ya muziki wa dansi
yenye makao yake kule Ujerumani.
Katika maonyesho ya kibiashara ya Afrika-Messe Trade fair kule mjini
Bremen,Ujerumani,bendi hiyo maarufu kwa kupelekana puta na washabiki
wake ilikutana na washabiki au wapenzi wa muziki walio gado katika
kuyarudi mangoma siku ya jumamosi 15.9.2012 mjini Bremen.
Ambako maonyesho hayo aliudhuriwa na maelfu ya watu,Ngoma Africa band
ndio walikuwa wakisubiriwa kwa hamu,walipanda jukwaani saa 11 alasiri
na kuanza kupeleka mashambulizi ya muziki kwa washabiki ambao waliupokea
mdundo kwa kila hali.
Wasikilize FFU katika kambi yao at www.ngoma-africa.com
wasiliana nao at contact@ngoma-africa.com
Kamanda wa FFU Ras Makunja akiongoza mashambulizi ya FFU
Ligwaride likiendelea Bremen
Gwaride jukwaani na dogo janja
Kikosi kizima cha FFU ughaibuni

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. wajamaa wanatisha,yaani wanatumia kila nafasi kuwakamua kisawa sawa ughabuni,kazeni buti ffu,mnakubalika
    Kimataifa

    ReplyDelete
  2. kazi ipo,naona ffu mmepania kushambulia kila kona

    ReplyDelete
  3. kamanda ? ndio kusema umehamua kukinusha kila kona

    ReplyDelete
  4. kamanda mkuu wa ffu,naona siku hizi umetulia sana,sikusikii vijembe vyako?
    au unaowarushia vijembe wamekuziba mdomo kwa vijisenti?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...