Meya wa Manispaa ya Ilala na Diwani wa kata ya Gongo la Mboto Mh. Jerry Silaa akimtwisha ndoo ya Maji, Bi. Hadija ambae ni mkazi wa mtaa wa Kilimo aliyoyachota kutoka katika kisima alichokikabidhi kwa wakazi wa mtaa huo leo.
 Mh. Jerry Silaa akimkabidhi seti ya vifaa vya michezo, mmoja kati ya manahodha wa timu zilizoshiriki ligi ya mpira wa miguu katika kata ya Gongo la Mboto ijulikanayo kama Jerry Super 8.
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala ambaye pia ni diwani wa kata ya Gongo la Mboto akizindua rasmi kisima cha maji kilichojengwa kwa ushirikiano wake na mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa Kilimo Bw. Moshi Mwaluko.
Baadhi ya wakazi wa kata ya Gongo la Mboto wakimsikiliza kwa makini Diwani wa kata yao Mh. Jerry Silaa (hayupo pichani), wakati akiwakabidhi vifaa vya michezo pamoja na kisima cha maji.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...