Mjomba, Aslaam aleikhum,
Katika kudumisha undugu wa jadi kati ya wananchi wa Tanzania na Malawi, Planet Darts club ya Kalonga (pichani) imetua nchini kwa  ziara ya mchezo wa kirafiki wa darts na Wanyambala wa Tukuyu  tangu Jumamosi 01/09/2012. Mechi itaanza muda wowote kuanzia saa 2 jioni ya leo. 
Wanyambala wapo fiti sana kwa mchezo huo japo wa Malawi nao wamejiandaa vya kutosha kwa wanasema hawatakubali kuchapwa mara mbili kwani mapema Julai mwaka huu walifungwa kwao Kalonga, Wanyambala walipo watembelea.

Leo ni patashik hapa Tukuyu nguo kuchanika. 
Matokeo yatatumwa kwa blog yetu mchezo ukimalizika.

Mjomba Juma
Tokyo

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Wakigombana ndugu chukua nyavu ukavue samaki!

    Wamalawi huu ndio undugu!

    Sio ule mpango wenu kama vile mnaotumiwa na watu kudai kuwa Ziwa nyasa lote ni la kwenu!

    Sasa wanandugu Darts mnatoka kwenu Karonga-Malawi mnakuja Tukuyu-Tanzania mchezo tunacheza wote lakini muda wa chakula mnataka wenzenu tusiwe na kitoweo cha samaki?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...