Waziri wa Uchukuzi akimkaribisha Naibu Waziri Mkuu wa China
Mhe. Hui Liangyu katika Station ya Mamlaka ya Reli ya Tanzania na
Zambia (TAZARA). Naibu Waziri Mkuu wa China alikuwa na Ziara ya
kuangalia Namna Station hiyo inavyofanya kazi. Serikali ya China
imetuma wataalamu kwa ajili ya kufanya utafiti wa namna ya kuboresha
Mamlaka hiyo.
Naibu Waziri Mkuu wa China Mhe. Hui Liangyu(Mwenye Tai ya
Bluu),akisalimia na baadhi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Reli ya
Tanzania na Zambia (TAZARA) mara baada ya kuwasilini kwenye stesheni
hiyo.
Waziri wa Uchukuzi,Dkt. Harrison Mwakyembe (aliyenyoosha
mikono)akiteta jambo na Uongozi wa Wizara ya Uchukuzi pamoja na Baadhi
ya Wakurugenzi wa TAZARA wakati wakimsubiri Naibu Waziri Mkuu wa
China, Mhe. Hui Liangyu aliyekuwa na ziara ya saa moja katika taasisi
ya Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia TAZARA. Kulia kwa Waziri ni
Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Mhandisi Omar Chambo na Kushoto kwa
Waziri ni Naibu Katibu Mkuu wa Uchukuzi,Bw. John Mngodo.
Bw. Miao Zhong mmoja wa watafiti waliotoka China akimuonyesha
Naibu Waziri Mkuu wa China Mhe. Hui Liangyu(kulia kwa aliyejishika
jicho) njia ya reli ilipoanzia kwa upande wa Tanzania. Naibu Waziri
Mkuu wa China alikuwa na ziara katika Mamlaka hiyo leo asubuhi.
Waziri wa Uchukuzi akisisitiza jambo kwa waandishi wa
Habari(hawapo pichani),kushoto kwake ni Katibu Mkuu wa Wizara ya
Uchukuzi,Mhandisi Omar Chambo na Kulia kwa Waziri ni Naibu Katibu Mkuu
Wa Wizara ya Uchukuzi,Bw.John Mngodo.
Naibu Waziri Mkuu wa China Mhe. Hui Liangyu(wa saba kutoka
kushoto),akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Wizara ya
Uchukuzi, baadhi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Usafiri wa Reli ya
Tanzania na Zambia (TAZARA) mara baada ya kuwasili katika station hiyo
leo asubuhi.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...