Meneja wa kinywaji cha Redd's Original,Victoria Kimaro (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu fainali ya Shindano la Redd's Miss Ilala 2012 inayotarajia kufanyika kesho ijumaa katika ukumbi wa Nyumbani Lounge,Namnga jijini Dar es Salaam.katikati ni Mratibu wa Shindano hilo,Juma Madabila na mwenye kofia ni Msanii wa Bongo Movie ambaye ndie atakaekuwa MC wa hafla hiyo,Steven Nyerere.wengine ni baadhi ya warembo wataoshiriki Shindano hilo la Redd's Miss Ilala 2012.
 Mratibu wa Shindano Redd's Miss Ilala 2012,Juma Madabila (katikati) akitoa taarifa ya Shindano hilo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa kutangaza burudani na zawadi kwa mshindi wa kwanza wa shindano hilo,ambaye atajinyakulia kitita cha Sh. Milioni 1.5.
Msanii wa Bongo Movie ambaye ndie atakaekuwa MC katika Shindano hilo,Steven Nyerere akielezea namna alivyojiandaa kuliendesha shindano hilo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...