Meneja wa kinywaji cha Redd's Original,Victoria Kimaro (kushoto) akizungumza
na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu fainali ya Shindano la Redd's Miss Ilala 2012
inayotarajia kufanyika kesho ijumaa katika ukumbi wa Nyumbani Lounge,Namnga jijini Dar es Salaam.katikati ni Mratibu wa Shindano hilo,Juma
Madabila na mwenye kofia ni Msanii wa Bongo Movie ambaye ndie atakaekuwa MC wa hafla hiyo,Steven Nyerere.wengine ni baadhi ya warembo wataoshiriki Shindano hilo la Redd's Miss Ilala 2012.
Mratibu wa Shindano Redd's Miss Ilala 2012,Juma
Madabila (katikati) akitoa taarifa ya Shindano hilo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa kutangaza burudani na zawadi kwa mshindi wa kwanza wa shindano hilo,ambaye atajinyakulia kitita cha Sh. Milioni 1.5.
Msanii wa Bongo Movie ambaye ndie atakaekuwa MC katika Shindano hilo,Steven Nyerere akielezea namna alivyojiandaa kuliendesha shindano hilo.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...