Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk. Emmanuel Nchimbi leo amepokea Ripoti ya Kamati
aliyoiunda mwezi uliopita kupata taarifa kuhusu vurugu zilizotokea Mkoani
Iringa ambazo zilisababisha kifo cha aliyekuwa mwakilishi wa Kituo cha Televisheni
cha Channel Ten, Daudi Mwangosi.
Vurugu
hizo zilitokea Septemba 2, mwaka huu katika Kijiji cha Nyololo, wilayani
Mufindi wakati Polisi walipokuwa wakiwatawanya wafuasi wa Chama cha Demokrasia
na Maendeleo (Chadema) waliokuwa wakifungua tawi la chama hicho katika kijiji
hicho.
Akikabidhi
Ripoti hiyo, Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo Bw. Theophil Makunga alisema
Kamati yake ilifanya ziara mkoani Iringa na kufanya mahojiano na wadau
mbalimbali na pia jijini Dar es Salaam.
Akipokea
Ripoti hiyo, Waziri Nchimbi aliishukuru Kamati hiyo kwa kazi waliyoifanya na
kusema yeye na Kamati hiyo watafanya kikao na Waandishi wa habari siku ya
Jumanne saa 4 asubuhi.
Imetolewa
na Isaac J. Nantanga
Msemaji
wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
06
Sept., 2012


iwekeni basi ripoti hapa tuione. kuna usiri gani tena wa kuficha ficha?
ReplyDelete