Mkurugenzi wa Kampuni ya kusambaza vipoza hewa (Air Condition) Unicool, Mohamed Rwenyemamu(kushoto) akimkabidhi zawadi ya kikombe na simu aina ya Sumsang Galaxy mshindi wa mashindano ya Unicool Monthly Mug kwa mwezi wa October ndugu Joseph Tairo.

=====  ======  ====

TAIRO BINGWA MICHUANO YA GOFU YA UNICOOL MONTHLY MUG

Mchezaji Joseph Tairo wa Dar Es Salaam Gymkhana ametwaa ubingwa wa michuano ya gofu ya Unicool Monthly Mug kwa kupiga mikwaju ya net 68 kwenye uwanja wa Lugalo jijini Dar Salaam mwishoni mwa wiki.

Mashindano hayo yaliandaliwa na klabu ya Lugalo chini ya udhamini wa kampuni ya Unicool inayojishughulisha na usambazaji wa vipoza hewa (Air Conditions). Baada ya kushinda, Tairo alisema mashindano yalikuwa mazuri na wachezaji wote walionyesha upinzani wa hali ya juu sana.

Nafasi ya pili katika mashindano hayo ilikwenda kwa Charles Sanga aliyepata net 77 kwa kumshinda Mkuu wa majeshi mstaafu George Waitara kwa c/b baada ya wote kupata net 77. Kwa upande wa wanawake mshindi alikuwa Amina Khamisi aliyeshinda kwa mikwaju ya netti 72, nafasi ya pili ikaenda kwa Sarah Denis aliyepata netti 73.

Kwa upande wa ‘Division A’ mshindi alikuwa Shabani Kibuna aliyeshinda kwa netti 68, nafasi ya pili ilichukuliwa na Abdallah Yusuph aliyepata netti 71 na ya tatu ikaenda kwa Brandy Mitchel aliyepata netti 77. Upande wa ‘Division C’ mshindi alikuwa Moses Amateku aliyeshinda kwa netti 66, nafasi ya pili alikuwa Mohamed Rwenyemamu aliyepata netti 71 na ya tatu akaenda kwa Ali Mfuruki aliyepata netti 72.

Mkurugenzi mtendaji wa Unicool, Mohamed Rwenyemamu alisema kuwa kampuni yake imeridhika na idadi kubwa ya wachezaji waliojitokeza kushiriki mashindano hayo kila mwezi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...